ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 20, 2017

MWILI WA MCHEZAJI MAARUFU WA NFL ALIYEJIUA GEREZANI WAKUTWA NA MSTARI WA BIBLIA ULIOANDIKWA KWENYE PAJI LA USO.

Mchezaji maarufu wa FNL Footballer  Aaron Hernandez, aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka ya mauaji ya mwaka 2015, amekutwa jana Jumatano (19 April) akiwa amekufa katika chumba chake cha gerezani ikisemekana kuwa amejinyonga kwa kutumia shuka lake za kulalia.

Hernandez aliyekuwa na umri wa miaka 27, hakuacha barua yoyote au kielelezo cha sababu za kujiua kwake, lakini inaripotiwa kuwa aliacha maandishi ya mstari wa biblia kwenye paji la uso wake yaliyoandikwa "John 3:16.

Mstari huo wa Biblia unasema "Kwa maana hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwana wake wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele." 

The Washington Post wanaripoti kuwa katika tukio hilo lenye maswali mengi Biblia imepatikana ndani ya selo yake ikiripotiwa kuwa wazi katika ukurasa huo wenye mstari tajwa.
Hernandez alikutwa na kosa la mauaji kupitia tukio la moja la mauaji ya klabu ya usiku nchini marekani ambapo watu walikuwa wakipigana naye kuingilia kati na katika hali hiyo mmoja kati ya waliokuwa wakipigana alikufa kwa kupigwa risasi na ikasemekana Hernandez ndiye aliye fyatua risasi hiyo.

Kesi iliendeshwa kwa muda wa miezi takribani tisa hadi kumi na hatimaye wiki mbili zilizopita makosa mawili yaliondolewa akabaki na makosa matatu kati ya makosa matano aliyokuwa akikabiliana nayo hata hivyo akaendelea kutumikia kifungo cha maisha gerezani.

Jana tarehe 19 Hernandez kapatikana akiwa amejiua ndani ya selo yake, tukio ambalo limezua utata na maswali mengi kwani askari magereza kwa upande wao wanadai kuwa hakukuwa na dalili zozote kwa marehemu kuwa na mpango wa kujitoa uhai wala kufanya tukio lolote la ajabu.

Maafisa wa Souza-Baranowski Correction Center in Shirley walijaribu kuokoa maisha ya Hernandez kwa kumkimbiza UMass-Memorial Health Alliance Hospital iliyoko mjini  Leominster ambako ndiko ilithibitishwa na madaktari kuwa alikuwa amefariki dunia at 4.07am.

Maelezo mengine toka kwa wakuu wa gereza wanasema wamemkuta akiwa amejinyonga ile hali akiwa amejifungia kwa ndani.

Utata umezuka toka kwa ajenti wa Hernandez ambaye pia ni mwanasheria wake aitwaye Jose Baez, akidai kuwa kuna mchezo mchafu umechezwa hapo, kwa sababu kuna mambo mengi yanaonekana kuwa hayajakaa vizuri akihoji "Kwanini ajiuwe kwa muda huu ambapo wiki mbili zilizopita alipatikana kuondoshewa baadhi ya makosa?" Kisha akaongeza "Na kulikuwa na uwezekano mkubwa kwamba huwenda kifungo chake kingelegezwa hapa kuna mbinu mbaya"

"Familia na timu yake ya uangalizi imeshtushwa sana na kushangazwa na taarifa za kifo cha Aaron" 

"Kulikuwa hakuna mazungumzo yoyote aliyofanya na mkewe, mwanawe, dada yake au hata familia yake zilizo ashiria hiki kutokea. Mara zote Aaron alikuwa akizungumza lugha ya matumaini kwamba kuna nafasi nyingine, nafasi yake kuudhihirishia ulimwengu kuwa yeye hakuhusika na mauaji yale" alisema Baez na kuongeza zaidi  "Wote tuliompenda na kumjali tumevunjika mioyo lakini tunasema lazima ukweli ujulikane juu ya kifo chake. Ni imani yetu mamlaka husika zitakusanya taarifa za ukweli kupitia uchunguzi watakaoufanya" alimaliza mwanasheria huyo.

On Friday (14 April), a Boston jury found Hernandez not guilty of the 2012 deaths of two men, Daniel de Abreu and Safiro Furtado. Hernandez was serving a life sentence after being convicted in 2015 of the 2013 death of semi-pro football player Odin Lloyd.

According to the Boston Globe, Hernandez may have died an innocent man in the state of Massachusetts due to an archaic legal principle known as "abatement ab initio". Hernandez was appealing his conviction and because he died before exhausting his legal appeals, his case would revert to its status at the beginning.

Hernandez's appellate attorney, John M Thompson, told the Globe he would file to vacate the conviction. That move could be challenged by the Bristol County District Attorney Thomas M Quinn III's office or the Lloyd family.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.