ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 21, 2017

WASANII MKOANI GEITA WAIOMBA SERIKALI KUWATAMBUA KATIKA SHUGHULI AMBAZO WANAZIFANYA.

Meza kuu ikiongozwa na mgeni rasimi ambaye ni afsa maendeleo wa halmashauri ya Mji ndugu,Maiga Majagi aliyevaa shati ya drafti katikakati.
Msanii wa nyimbo za asili katoka kata ya Bukoli akiburudisha wakati wa mashindano hayo.
Mwenyekiti wa chama cha wasanii Mkoani Geita,Rose Bonface (ROSE BONANZA) akitambulisha baadhi ya wageni waalikwa.
Moja kati ya majaji katika mashindano hayo,Bi Anithar Kagemulo akijitambulisha wakati wa mashindano hayo.
Kikundim cha uwimbaji kutoka wilayani Chato cha Mwagazege kikiimba katika mashindano hayo.
Mgeni rasimi ambaye ni afsa maendeleo ya jamii Ndugu Maiga Majagi akizungumza na wasanii huku akiwaasa kuendeleo kuwa na umoja na kushikamana ili kuendeleza sanaa katika Mkoa wa Geita.
Meza kuu ikimsikiliza mgeni rasimi wakati wa hotuba yake .
Majaji wakifatilia mashindano.


PICHA NA JOEL MADUKA

STORY NA MADUKAONLINE

GEITA:Chama cha wasanii Mkoani Geita,kimeiomba serikali Mkoani humo kuendelea kutoa ushirikiano katika Nyanja hiyo muhimu ikiwa ni pamoja na kusapoti kazi  ambazo zimekuwa zikifanywa  na wasanii.

Kauli hiyo imesemwa na mwenyekiti wa chama hicho Mkoani Humo Rose Bonface wakati wa ufunguzi wa mashindano ya kuwasaka wasanii wenye vipaji vya kuimba kuigiza na kuchekesha yaliyokuwa yanafanyika katika ukumbi wa halmashauri ya Mji wa Geita.

Rose alisema kuwa Tasnia ya sanaa bado inachangamoto nyingi ikiwa ni pamojan na kushindwa kutambulika na kushikwa mkono  kwenye serikali kutokana na kwamba baadhi  viongozi wa kiserikali wanaona swala la wasanii limekaa kiunu jambo ambalo si kweli kwani  kazi ya sanaa ni sawa na shughuli zingine katika jamii.

“Sisi wasanii bado tunachangamoto kubwa sana katika serikali ingawa kwa sasa kuna wizara inayotutambua lakini bado kuna ugumu mwingi tu tukiangali kwenye serikali kuna viongozi ambao wanaona kuwa hatuna mchango wowote lakini sio kweli sisi tunauwezo wa kufikisha ujumbe kwa jamii na ikatuelewa zaidi kuliko vile ambavyo serikali imeendelea kutuchukulia”alisema Rose.

Kwa upande wake mwenyekiti wa waigizaji Mkoa wa Mwanza,Ramadhani  Masululi,amesema kuwa jambo ambalo limekuwa likisababisha sanaa au wasanii kuonekana ni wahuni ni kutokana na baadhi ya wasanii kuonekana kutokujieshimu na wengine kuingia kwenye sanaa bila ya kuwa na maono au mtazamo chanya katika sanaa.

“Sanaa sio uhuni kwanini wanasema uhuni waigizaji  wengine wameingia ni mamluki unakuta mwingine anaingia kwenye sanaa ni mlevi mvuta bangi na mwingine ni Malaya na hii ya wezekana kwasababu nikutokana na vigezo kutokuwa vigumu lakini sisi kama chama  cha wasanii hatuwezi kukubaliana na swala hili tutaakikisha wale wenyetabia za ajabu wanatupisha ili tuwe na wasanii ambao wananidhamu”alisema Ramadhani

Akimwakilisha Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Geita ambaye ndiye alikuwa mgeni rasimi kwenye uzinduzi huo,afisa maendeleo ya jamii wa halmashauri hiyo,Maiga Majagi,amewaasa wasanii kutumia umoja wao  kuleta mabadiliko kwa wanageita kwa kufanya kazi na kukitumia chama chao kwa kuwa tetea zaidi na kupata taarifa  mbali mbali za soko la kazi zao na pia amewataka  kupanga mikakati ya kushirikiana  na wadau wote  na kwamba jambo likiongelewa na wote linakuwa na nguvu kuliko kuzungumziwa na mtu mmoja.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.