ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 24, 2016

ASKARI POLISI WILAYA YA RORYA WALALAMIKIWA KWA KUNYANYASA WANANCHI NA BODABODA.

Askari wanapopata fedha za waendesha badaboda hufanya tendo la kugawana na hata kudiliki kununua bidhaa kwa fedha ambayo wameipata kwa mazingira yenye kunyanyasa bodaboda na wananchi kwenye maeneo ya magulio, minada na masoko maeneo mbalimbali ya Kata za Jimbo la Rorya kama walivyonaswa na camera yetu  hivi karibuni maeneo ya gulio na mnada wa Nyamaguku.
2
3
4
5
6

 Na Peter Fabian, RORYA.

ASKARI Polisi wa Kanda maalumu ya Tarime na Rorya waingia matatani ni baada ya kudaiwa kuwanyanyasa wananchi wa baadhi ya maeneo ya Kata za Jimbo la Rorya Mkoa wa Mara wanapokwenda kwenye magulio na minada ya mifugo huwavizia maeneo ya porini na kuwakamata na kuwashikilia hadi wanapotoa fedha ndipo huwaachia .

Wakizungumza na GSENGO BLOG kwa nyakati katika maeneo ya Kata za Shirati, Utegi, Labwoli, Kumuge, Kisumwa, Nyamuga wakiomba kuhifadhi majina yao kwa kuhofia kukamatwa na askari Polisi wamelalamikia kuwepo kero hiyo na unyanyasaji unaofanywa na askari hao hasa siku za magulio na minada ya Nyamaguku, Shirati, Mtana na Randa.

Ni askari wa Trafiki na Polisi kutoka Kituo cha Polisi Shirati wakiwa wamezingilwa na wananchi na waendesha pikipiki baada ya kuzikamata bodaboda zao na kuzishikilia huku ikidaiwa kuwatoza fedha kwa nguvu bila kuwapatia stakabadhi (risti) iwapo walibainika kuwa na makosa ambapo utaratibu hutozwa faini na kuandikia stakabadhi badaboda hao, lakini sasa ni tofauti imedaiwa kuwa ni kero na unyanyasaji kwa badaboda katika magulio, masoko na minada ya mifugo maeneo ya Shirati, Nyamaguku, Utegi, Randa, Mtama Jimbo la Rorya, umedaiwa kugeuzwa mradi wa kujipatia fedha, badaboda huwafukuza kwa gari la OCD Utegi, OCD Shirati na OCD Kinesi wa Kanda Maalum ya Tarime na Rorya huku askari Polisi wa kawaida wao hutumia pikipiki kuwafukuza hadi porini na huwapiga wanapowakamata na huwasababishia ajari na kuwaacha wakiwa majeruhi kama walivyonaswa na camera yetu hivi karibuni huko Shirati.
“Siku ya gulio na mnada wa mifugo katika maeneo ya Nyamaguku, Shirati, Mtana na Randa wananchi, wafanyabiashara  na waendesha pikipiki (bodaboda) askari polisi huja kwa wingi wakiwa na silaha kwenye pikipiki (bodaboda) sita wakiwa wamebebana wanazokuwa wamezikamata kwa wananchi na wengine kwenye magari ya Polisi PT 1691ya Kanda maalumu Tarime na Rorya na PT ya OCD Utegi,”alieleza mmoja wa wananchi.

Aidha mmoja wa wananchi hao alieleza kwamba askari hao wamekuwa wakivizia siku za magulio, minada na masoko ambapo huwaja kwa wingi na wamekuwa na tabia ya kuwaamusha usiku wa kuanzia saa 10:00 alfajiri hadi saa 2:00 asubuhi wakidai wanasaka nyavu haramu na samaki wachanga na wakikosa huwavizia badaboda na kuwafukuza kwa gari na pikipiki hadi wawapatie fedha.

“Hii ni kero kubwa kwa vijana waendesha bodaboda na wananchi wanaotumia usafiri huo umeonekana kuwa ni mradi wa askari Polisi wa Kanda Maalumu ya Tarime na Rorya ambao wamekuwa wakiwakamata na kuwaomba fedha na wanapokosa huwaomba hadi kuku na hata wanapodai stakabadhi (risti) huambiwa kwa kufokewa huku wakitishiwa pikipiki zao kwenye magari,”alisema Kiongozi wa bodaboda mmoja.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Rorya Mkoa wa Mara, Lameck Airo (CCM), aliwaeleza waandishi kuwa amekuwa akipata malalamiko ya wananchi na viongozi wa vijiji na Kata kuwepo kwa maaskari wanaowanyanyasa na kuwakamata waendesha bodaboda kwa kuwavizia maeneo ya porini na kuwakamata kisha kuwatoza fedha hadi kuwaomba kuku na mbuzi bila kuwambia makosa yao.

“Nimekuwa nikikutana na Wakuu wa Polisi kila mara na hata kumueleza Kamanda wa Kanda Maalumu ya Tarime na Rorya (RPC) Andrew Sata lakini hali hiyo husitishwa kwa muda wa wiki moja hadi mbili lakini huibuka kwa nguvu kubwa na hii imekuwa kero kwa wananchi na hasa bodaboda kweli wananyanyasika kwa kukamatwa na kuombwa fedha zisizokatiwa stkakabadhi,”alisema.

Mbunge Airo ameeleza kuwa kufatia hatua ya wananchi hao kulalamika atalifikisha suala hilo kwa IGP, Ernest Mangu na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba pamoja na uongozi wa Serikali Mkoa wa Mara kwa kuwa askari hao katika baadhi ya vituo wamekuwa wengi zaidi ya mahitaji ambapo alitolea mfano wa Kituo cha Kinesi kina sakari zaidi ya 100 ambao kazi kubwa kwao ni kutafuta fedha kwa wananchi.

“Tunashukuru askari Polisi waliokuwa wameletwa kwa wingi wakati wa kuanzishwa Kanda maalumu kwa lengo la kuzuia wizi wa mifugo na mapigano ya wakurya na wajaluo wakati ule ambapo walisaidia sana na kumaliza lakini sasa wameonekana askari hao kuwa kero ya kunyanyasa wananchi kwa vitendo hivyo na hili linahitaji askari hao wapelekwe kwenye mahitaji,”alisisitiza.

Naya Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Tarime na Rorya (RPC), Andrew Sata alipotafutwa kwa njia ya simu alisema kwamba taarifa hizo ndo kwanza anazisikia na kuomba alifanyie kazi suala hili na kisha atalitolea taarifa na kwa sasa hawezi kulizungumzia kwa kuwa ni kipindi cha sikukuku na kazi kubwa ni kuimalisha ulinzi katika maeneo mbalimbali ya Kanda hiyo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.