ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 26, 2016

CHAMELEONE AVUNJA NDOA YA WATU UGANDA.

Mwanamke nchini Uganda amepewa talaka baada ya kulia jina la Chameleone wakati akishiriki mapenzi na mumewe

– Chameleone ameweka kisa hicho kwenye Instagram baada ya kuchapishwa na gazeti moja la Uganda

Mwanamke mmoja Uganda amepewa talaka baada ya kuliita jina la msanii msifika Jose Chameleone wakati wakishiriki mapenzi na mumewe.

Habari hizo zimeenea kote Uganda baada ya mume huyo kuapa kumfurusha mkewe alipomlia mwimbaji huyo wa kibao maarufu Valu Valu.
Msanii wa Uganda Jose Chameleone. Picha: Instagram/jchameleone

Chameleone alionekana kufurahishwa na tukio hilo kiasi cha kupiga picha za habari zenyewe kwenye gazeti moja la hapo.

“Mume amfukuza mke kwa kumite Chameleone wakati wakishiriki mapenzi,” msanii huyo aliandika kwenye maelezo ya picha hiyo.

Kisa hicho kinajuia siku chache tu baada ya mwimbaji huyo maarufu wa Uganda kushirikiana na kundi la Elani katika kolabo ya “My Darling”, wimbo unaoangazia mapenzi, changamoto na kutoelewana kunakowakumba wapenzi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.