ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, June 28, 2016

FELLA ATOA KAULI YA WCB’ BAADA YA DIAMOND KUKOSA TUZO YA BET.

Kutoka kushoto ni Babu Tale, Diamond na Fella.

Mmoja kati ya viongozi wa juu wa label ya WCB, Mkubwa Fella amesema kuwa WCB imekubali kilichotokea katika tuzo za BET licha ya kukiri kwamba walikuwa wana matarajio makubwa ya kuchukua tuzo hiyo ambayo ilikuchuliwa na Black Coffee kutoka Afrika Kusini.

Akiongea na Redio 5 ya Arusha Jumatatu hii, Fella amezungumzia matokeo hayo pamoja na kwanini walikuwa namarajio makubwa.

“Tumepokea vizuri sana kwa sababu mwisho wa siku ni msanii pekee wa Kitanzania,” alisema Fella “Msanii wa kitanzania kuingia kwenye tuzo kama hizo ambazo ni kubwa duniani bado tunaona tunanafasi ya kufanya mazuri zaidi,”

Aliongeza, ‘Hatuwezi sema tulikosea kwa sababu mwisho wa siku yale ni mashindano kwamba mmoja lazima achukue, kwa hiyo Black Coffee alichofanya ulimwenguni kimemeona ni bora, yeye ni bora, kwa hiyo na sisi Watanzania tutengeneze vitu bora kama vya wenzetu,”

Pia kiongozi huyo alisema walikuwa na matarajio ya kuchukua tuzo hiyo.

“Hata ukiniambia leo nikapigane na Tyson na uhakika wa kupigana naye na nikashinda, sina maana kwamba naenda kupigana na Tyson ndio nikapigwe,”

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.