ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, June 16, 2016

AIRTEL YAENDELEA KUWAPATIA WATANZANIA SIMU ZENYE UHALISI.

Maafisa wa Airtel watitoa maelekezo kwa Wateja kutokana na ofa kabambe za “simu za bure na halisi" zinazopatikana katika maduka Airtel, ambapo leo hii Airtel wapo maeneo ya mnazi mmoja katika ofisi za halmashauri ya manispaa ya Ilala, ambapo wiki ijayo wataendelea kuwepo katika ofisa za halmashauri ya manispaa ya Ilala na Kinondoni.

Airtel yaendelea kuwapatia watanzania simu zenye uhalisi.
• Simu za Bure katika maduka ya Airtel nchi nzima
• Vifurushi vinavyodumu kwa miezi minne na dakika zaidi ya 1000
Dar Es Salaam, 16 Juni 2016, Kufuatia tamko la serikali la kuzima simu zote bandia ifikapo tarehe 16 Juni 2016, Airtel Tanzania imeendelea kutoa ofa kabambe za “simu za bure na halisi" zinazopatikana katika maduka yote ya Airtel nchi nzima. Tangazo hilo limesema kwamba simu za Bure na halisi zinapataikana kwa wateja wote wenye simu bandia na  ambazo sio za viwango vinavyokubalika  katika soko la Tanzania  , kwa kununua kifurushi chenye dhamani  ya sh. 22,000 / = Tshs tu.   Simu hizi za bure na halisi zinazotolewa  na Airtel ikiwemo  ITEL 2090 na FERO 180, zikiwa na dakika  550  kwa kupiga mitandao yote, zenye ujumbe mfupi 3000 na 250 MB kwa muda wa miezi minne.

 Akitoa maoni yake juu ya ofa hii, mkuu wa kitengo cha  Internet Airtel Tanzania, Gaurav Dhingra alisema "kwakutambua kwamba baadhi ya wateja wetu  bado wanatumia simu ambazo hazina uhalisia, tumeendelea kufanya jitihada za kuwapatia simu halisi.Napenda kusisitiza kuanzia kesho kwa wale  wenye simu zitakazo zima leo usiku wasi hofu kwani laini zao hazitahadhirika na vifurushi na pesa ndani ya simu zao zitaweza kutumika pale watakapo nunua simu zenye kiwango kinachokubalika kwenye maduka yetu nchi nzima kwa kupata simu halisi, na vifurushi vitakavyo dumu kwa miezi mine

Le tupo maeneo ya mnazi mmoja katika ofisi za halmashauri ya manispaa ya Ilala, ambapo wiki ijayo wataendelea kuwepo katika ofisa za halmashauri ya manispaa ya Ilala na Kinondoni.  Dhingra aliendelea kufafanua kuwa, ili kuwapa wateja wetu uwezo wa kuchagua simu zinazokidhi mahitaji yao ,tumeongeza simu za aina mbalimbali ikiwemo Magnus Z11, Huawei Y3C na Techno W3  ambapo mteja akinunua anapata kifurushi chenye dakika zaidi ya 1000 . "Tunatoa wito kwa wateja wetu wa Airtel wenye simu bandia kufika kwenye duka letu lolote la Airtel na simu yake ili ajipatie  simu yenye kiwango kinachokubalika kwa gharama nafuu zaidi kwa kununua kifurushi cha Airtel na kupata simu bure. "alinukuliwa Dhingra

Wateja wa Airtel wanaweza kuhakikisha kama simu zao ni bandia au la, kwa kupiga *#06# au kutembelea mawakala katika maduka ya Airtel lililokaribu nae.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.