ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 26, 2016

AIRTEL MONEY YAWEZESHA KUBETI NA KULIPA KWA AIRTEL MONEY

Meneja wa Airtel Money, Asupya Naligingwa (kushoto) akiongea wakati wa kuzindua ushirikiano kati ya kampuni ya Airtel na M-bet utakaowawezesha wapenzi wa kubashiri michezo mbalimbali kubaashiri na kisha Mr. Money kuwawezesha kulipia kupitia huduma ya Airtel Money. pichani ni Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando  katikati) akifatiwa na Mkurugenzi wa M- bet Dhiresh Kaba
 Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando  (katikati) akifafanua jambo kwenye huma hizo.\
Mkurugenzi wa M- bet Dhiresh Kaba (kushoto) akipongezana na Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando (kulia) mara baada ya kuzindua ushirikiano utakaowawezesha wateja watakaobashiri michezo mbalimbali na kisha Mr. Money kuwawezesha  kulipia kwa kutumia huduma ya Airtel Money. akishuhudia ( nyuma kushoto) ni Meneja wa Airtel Money , Asupya Naligingwa
MR MONEY WA AIRTEL AJA NA SULUHISHO LA MALIPO WANAOBET MICHEZO KUWA SALAMA

Mr.  Money awawezesha wateja wa Airtel wanaobet kufanya malipo kwa Airtel Money
Dar es salaam 25 mei 2016 Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeshirikiana na kampuni ya M- bet na kuwawezesha wateja wa M-bet kubashiri michezo wa mpira wa miguu ikiwemo ligi E Premier League, Laliga,Bundesliga, Serie A  kisha  kufanya malipo kwa urahisi na usalama kwa kupitia huduma ya Airtel Money

M- Bet ni kampuni inayowawezesha wateja wake kubashiri mshindi katika michezo mbalimbali ya soka duniani kote.

Akiongea wakati wa kutangaza ushirikiano huo Mkurugenzi wa M-Bet Mr. Dhiresh Kaba alisema “Mr Money wa Airtel Money ametupatia suluhisho la kupokea malipo na kulipa wateja wetu ushindi wao kwa usalama zaidi, hili limekuja wakati sahihi kwa kwa kuwa sasa tunaelekea msimu mpya wa ligi za mpira wa miguu hasa ligi ya Uingereza ambapo  wanaobashiri wataweza kubashiriri wakiwa popote na kufanya malipo bila ya kuwa na haja ya kutembelea ofisi za M-Bet kwa urahisi na usalama”

Ili kuweza kufurahia huduma hii unachotakiwa kufanya  tembelea tovuti ya m-bet www.m-bet.co.tz,   pakua  program ya m-bet App.net. Tabiri na ushinde na m-bet.  Mshindi anaweza kushinda hadi shilingi mil 10.  Ili uweze kukamilisha malipo yako huhitaji kubeba pesa tasilimu tena badala yake fanya malipo kwa njia salama ya Airtel Money kwa kupiga  *150*60# kisha chagua namba 5 malipo au(lipia bill) alafu chagua namba 3 weka namba ya kampuni 300300 na kuweka kumbukumbu namba yake. Aliongeza Mr. Dhiresh Kaba wa M-Bet

Kwa upande wake Meneja wa Airtel Money Mr. Asupya B. Nalingigwa alisema”Mr, Money anaendelea kudhihirisha kauli yake ya kwamba yeye ni nafuu na uhakika pale unapotaka kufanya malipo, leo uzinduzi huu wa kulipia tozo za kubashiri/kubet kwa Airtel Money itasaidia kuwaepusha wateja wanaoshiriki mchezo huo wa kubet/kubashiri  majanga ya kutembea na burungutu la pesa taslim kwa kuwa ni salama zaidi.

Nalingigwa alisisitiza kuwa Mr. Money wiki iliyopita alitangaza huduma pekee zinazotolewa na Airtel Money ikiwemo mikopo ya Timiza, nyongeza ya Uniti ukinunua LUKU kwa Airtel Money, nyongeza ya muda wa maongezi au vifurushi kwa Airtel Money bado Mr Money anaendeleza kuweka suluhisho kwa kila mahitaji, bidhaa na huduma mbalimbali”.

“ni uhakika kuwa Mr Money sasa atapokea malipo ya wewe unaebashiri na kisha atakulipa pesa ya ushindi wako wakati wowote mara baada ya kuthibitiishwa kuwa wewe ni mshindi na utaitoa kwa WAKALA  yoyote wa Airtel alisisitiza Bw, Nalingigwa

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.