ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, February 1, 2016

GUARDIOLA AKIOTESHA NYASI KIBARUA CHA PELLEGRINI.

Mhispania Pep Guardiola ametia saini mkataba wa miaka mitatu kuwa meneja mpya wa Manchester City baada ya msimu huu kumalizika.
Guardiola, atachukua majukumu hayo kuanzia Julai, klabu hiyo ya Ligi ya Premia imetangaza.
Manuel Pellegrini ataondoka klabu hiyo Juni 30 baada ya kumalizika kwa msimu wa sasa.
"Kutokana na heshima yetu kwa Manuel Pellegrini na wachezaji, klabu ingependa kufanya wazi uamuzi wake ili kuondoa nafasi ya uvumi,” City wamesema kupitia taarifa kwenye tovuti yao.
"Manuel, ambaye anaunga mkono kikamilifu uamuzi wa kufanya tangazo hili, anaangazia kutimiza malengo yake ya msimu huu na anadumisha kujitolea na heshima ambayo amekuwa nayo machoni ma wote wanaohusika katika uongozi wa klabu.”

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.