ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 25, 2015

SERIKALI YA CCM YAAHIDI UMEME VIJIJI VYOTE TANZANIA NDANI YA MIAKA MI 2 MADARAKANI.


Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wanachama wa CCM pamoja na wananchi wa Jimbo la Kilindi kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni Mkoa wa Tanga. Miongoni mwa ahadi aliyoitoa kwa wanaKilindi ni kulishughulikia suala la upatikanaji wa huduma za maji safi na salama pamoja na ujenzi wa barabara ya kuingia na kutoka katika Wilaya hiyo.

Baadhi ya wananchi na wanachama wa CCM Kijiji cha Kwediboma wakiwa wamesimamisha msafara wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan kuwasikiliza kilio chao alipokuwa akisafiri kuelekea Wilaya ya Kiteto. Baadhi ya ahadi aliyoitoa Bi. Samia ni pamoja na upimaji wa ardhi ya vijiji na wilaya ili kumaliza migogoro ya ardhi kwa wafugaji na wakulima.  
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga akizungumza na wanaCCM na wananchi katika mkutano mdogo wa kampeni wa mgombea mwenza wa nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan uliofanyika Kilindi, Tanga.
Mgombea ubunge wa CCM Jimbo la Chemba, Juma Nkamia akizungumza na wanaCCM na wananchi katika mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa nafasi ya urais wa chama hicho, Bi. Samia Suluhu Hassan Wilaya ya Chemba. Miongoni mwa ahadi kwa wakazi wa eneo hilo alizozitoa ni kushughulikia migogoro ya ardhi suala la ukame na huduma za maji.
Kutoka kulia ni mgombea ubunge wa Jimbo la Kilindi, Mboni Muhita akiserebuka na baadhi ya viongozi na makada wa CCM walioongozana kwenye kampeni za mgombea mwenza Wilaya ya Kilindi.
Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan (kulia) akimtambulisha mgombea ubunge wa Jimbo la Kilindi, Mboni Muhita kwa wanachama wa CCM pamoja na wananchi wa Jimbo la Kilindi kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni Mkoa wa Tanga.

Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan (kulia) akionesha nakala ya ilani ya chama hicho kwa wananchi kabla ya kumkabidhi, mgombea ubunge wa Jimbo la Kilindi, Mboni Muhita kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni Mkoa wa Tanga.
Mgombea ubunge wa Jimbo la Kilindi, Mboni Muhita akionesha kwa wananchi nakala ya ilani ya uchaguzi ya chama hicho mara baada ya kukabidhiwa na mgombea mwenza kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni Mkoa wa Tanga.
Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan akimtambulisha mmoja wa wagombea wa udiwani CCM katika mkutano wa hadhara Jimbo la Kilindi.
Baadhi ya wananchi na wanachama wa CCM Kijiji cha Kwediboma wakiwa wamesimamisha msafara wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan kuwasikiliza kilio chao alipokuwa akisafiri kuelekea Wilaya ya Kiteto. 
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kampeni za CCM Taifa, Ummy Mwalimu (kushoto) na Mahadhi Juma wakijadili jambo kwenye moja ya mikutano ya kampeni ya mgombea mwenza. 

Aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Nkenge, Asumpta Mshama akizungumza na wanaCCM na wananchi katika mkutano wa hadhara Jimbo la Kilindi kunadi ilani ya CCM.
Baadhi ya wananchi wakiwa wamesimama juu ya kisiki kuweza kumshuhudia mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akiwasili Jimbo la Kilindi.
Baadhi ya wananchi na wanachama wa CCM Kijiji cha Kwediboma wakiwa wamesimamisha msafara wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan kuwasikiliza kilio chao alipokuwa akisafiri kuelekea Wilaya ya Kiteto. 
Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan akivishwa skafu kwa heshima na vijana wa UVCCM mara baada ya kuwasili katika Wilaya ya Kiteto ambapo alifanya mikutano ya kampeni kunadi ilani ya CCM. 
Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika ofisi za CCM Wilaya ya Kiteto kabla ya kuanzamikutano ya kampeni kunadi ilani ya CCM. 
Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wanachama wa CCM pamoja na wananchi wa Jimbo la Kiteto kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni Mkoa wa Manyara. Katika ahadi zake alisema ndani ya miaka miwili baada ya kuingia madarakani watahakikisha umeme unawaka katika vijiji vyote vya Tanzania.
Mgombea ubunge wa CCM Jimbo la Kiteto, Emmanuel Papian John (kushoto) akitambulishwa kwa wananchi na WanaCCM na Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan.
Sehemu ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Chemba, Wilaya ya Chemba.
Mgombea ubunge wa CCM Jimbo la Chemba, Juma Nkamia akizungumza na mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jimboni humo.
Mgombea ubunge wa CCM Jimbo la Chemba, Juma Nkamia (kulia) akizungumza na wanaCCM na wananchi katika mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa nafasi ya urais wa chama hicho, Bi. Samia Suluhu Hassan Wilaya ya Chemba. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma, Adam Kimbisa.
Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwenye mkutano wa hadhara Jimbo la Chemba.
Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wanachama wa CCM pamoja na wananchi wa Jimbo la Chemba kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni Wilaya ya Chemba. Picha zote na www.thehabari.com.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.