ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 8, 2015

JE! FAINALI NI JUVENTUS VS BARCELONA UEFA??


Juventus vs Real Madrid 2015 1-2 Goles Resumen All Goals And Highlights Champions League.

LIGI ya Mabingwa Ulaya UEFA imeendelea katikati mwa juma hili mchezo wa kwanza ukipigwa nchini Italia ukizikutanisha Juventus dhidi ya Real Madrid ambapo Juve iliondoka na ushindi mwembamba wa mabao 2-1.

Ule mchuano mkali wa kutupia gozi nyavuni kati ya Lionel Messi dhidi ya Cristiano Ronaldo umeendelea, kwani baada ya mchezo wa awali ulioshuhudia Ronaldo akifunga bao la kwanza la kusawazisha kabla ya kuongezwa jingine na matokeo kuwa 2-1, Lionel Messi aliibuka shujaa katika mchezo wa pili akijibu mapigo kwa kufunga magoli mawili kwenye mchezo wa nusu fainali ya pili dhidi ya Bayern Munich.

A riveting subplot has developed in this season's UEFA Champions League. The two greatest forwards of the age have both surpassed Raúl González's total for goals in the competition and after the first legs of the semi-finals, Lionel Messi leads Cristiano Ronaldo 77-76 having briefly fallen behind on Tuesday night.

Licha ya kufungwa katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza Real Madrid bado wana nafasi ya kusonga mbele hatimaye kutinga fainali wakihitaji ushindi wakuanzia bao 1-0 au bao 3-1 katika mchezo wa marudiano watakaocheza nyumbani kwao.

Upande wa pili Baryen Munich wanakibarua kigumu kubadili matokeo kwani kuifunga Barcelona iliyokamilika bao 4-0 kunahitaji miujiza.

Zaidi ya fainali Swali linabaki kuwa Je! nani atatengeneza historia kuwa mpachikaji mabao bora wa zama hizi? Ni Ronaldo au Messi? 


Barcelona vs Bayern Munich 3-0 2015 - All Goals 06-05-2015.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.