ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 8, 2014

HATIMAYE MISS TANZANIA 2014 SITTI MTEMVU ALIVUA RASMI TAJI, MSHINDI NAMBA MBILI AULA.

Taarifa tunazozipata sasa hivi kupitia Breaking News ya Clouds Fm iliyotoka katika kipindi cha Club 10 na Wewe, inasema kuwa Miss Tanzania 2014-2015 Sitti Mtemvu ameamua kulivua taji hilo rasmi mara baada ya kuandamwa sana na vyombo mbalimbali vya habari sambamba na mitandao ya kijamii.

Mpango huo wa kulivua taji utamnufaisha mshindi wa pili Lillian Kamazima, ambaye ndiye atakaye kuwa mrithi wa Taji hilo sanjari na zawadi zitakazo rudishwa na Sitti.

Taarifa hizo zinaendelea kusema kuwa mnyange huyo hivi sasa yuko katika ukumbi wa JB Belmonte jijini Dar es salaam akikamilisha hatua hiyo ambayo ni kwa mara ya kwanza imetokea ndani ya Historia ya Miss Tanzania.. (ZAIDI BOFYA PLAY KUSIKILIZA) ITAENDELEA....
TOP 3: Mrembo, Sitti Abbas Mtemvu, akiwa katika picha ya pamoja na Mshindi wa pili, Lillian Kamazima (kulia) na Mshindi wa Tatu, Jihhan Dimachk, baada ya kutawazwa rasmi kuwa washindi katika shindano la Taifa lililofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam,. Mrembo huyo ambaye ni binti wa Mbunge wa Temeke, pia ni Miss Temeke Abbas Mtemvu alitokea  Kitongoji cha  Chang'ombe hii leo ametangaza kulitema taji hilo.

HABARI HII TAENDELEA HIVI PUNDE.......

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.