ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 11, 2014

VIAGRA HUSABABISHA UPOFU

CHANZO:BBC SWAHILI
Watafiti nchini Australia wanadai kwamba dawa inayotumiwa kuongeza nguvu za kiume VIAGRA husababisha upofu baada ya mda mrefu.
Kulingana na Watafiti hao kutoka Australia, kiungo fulani katika dawa hiyo inayotumiwa kukabiliana na ukosefu wa nguvu za kiume,huathiri uwezo wa kuona miongoni mwa wanaume ambao wana ugonjwa wa macho.
Kulingana na gazeti la Nation nchini kenya, Madaktari nchini Australia wamebaini kwamba kiungo fulani katika dawa hiyo kinaweza kusababisha upofu miongoni mwa wanaume wenye tatizo la ugonjwa wa macho.
Vilevile inadaiwa kuwa dawa hiyo pia inaweza kuwaathiri watumiaji ambao wanaona vizuri.
Utafiti huo uliofanywa katika panya,ulibaini kwamba hata watu wasio na ugonjwa wa macho wanaweza kuathirika.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.