ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 23, 2014

WAZIRI MKUU PINDA ATEMBELEA UJENZI WA UPANUZI WA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA MWANZA LEO

Waziri Mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda (katikati), Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk Charles Tizeba (kulia mbele), Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarist Ndikilo (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Dkt Anthon Dialo (kulia kwa Pinda) wakiwa tayari wamevalia vifaa tayari kutembelea eneo la mradi wa ujenzi wa jengo la kuongozea ndege lililopo kilimani jirani na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwanza.
Waziri Mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda (wa pili kushoto), Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk Charles Tizeba (wapili kulia), Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto), Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Dkt Anthon Dialo (katikati), Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Amina Masenza, wakati Pinda wakieleza jambo wakati alipotembelea eneo la mradi wa ujenzi wa jengo la kuongozea ndege lililopo kilimani jirani na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwanza.
Watu wa Kazi za ujenzi wa jengo hilo.
Kutoka kilimani.
Mwonekano wa uwanja wa ndege wa Mwanza.
Ndege ya Air Tanzania ikituwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwanza
Waziri Mkuu Pinda akipata maelezo kutoka kwa Naibu Waziri wa Wizara wa Uchukuzi Dk Tibeza kilimani lilipo jengo la kuongozea ndege alipotembelea leo jijini Mwanza wengine ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Dkt Anthon Dialo (wa tatu kushoto), Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto mbele) wakiangalia uwanja wa ndege ambao kwa sasa uko kwenye upanuzi. 
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ilemela Zuberi Mbyana akiwa na Mkandarasi mshauri raia wa Zimbabwe.
Shehena ya changalawe zikiwa zikisubiria kuwekwa kwenye Mtambo wa kisasa kabisa wa kuchanganyia lami ya uwanja wa ndege wa Mwanza.
Mtambo wa kisasa wa kuchanganyia lami 
Waziri Mkuu Pinda akipata maelezo kutoka kwa Naibu Waziri wa Wizara wa Uchukuzi Dk Tibeza wakiangalia mtambo wa kisasa jana jijini Mwanza wengine ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Dkt Anthon Dialo (wa pili kushoto), Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto mbele) na kulia ni Mkandarasi wa ujenzi wa uwanja akitoa maelezo.
ulinzi umeimalishwa eneo alilotembela Waziri Mkuu Pinda.
Waziri Mkuu Pinda akipata maelezo ya Mkandarasi kwenye eneo linaloongezwa la urefu wa mita 400 la kurukia ndege kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwanza jana
Waziri Mkuu Pinda akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa ujenzi wa uwanja wa ndege na viongozi wengine.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.