ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, June 11, 2014

VURUGU ZA WAMACHINGA MWANZA MABOMU YA MACHOZI YARINDIMA ZAIDI YA SAA 3, BIASHARA ZAFUNGWA KABISA.

Jeshi la wananchi lilitoa askari wake wa kijeshi “MP” kuimarisha ulinzi kwenye vitengo vya mabenki, ofisi za serikali na maeneo nyeti ili kutokwaza shughuli za kila siku kuendelea.
KATIKATI ya jiji la Mwanza leo paligeuka kuwa pachungu baada ya mabomu zaidi ya 120 kulindima toka saa 3:58 asubuhi hadi 8:45 na kulifanya eneo hilo lisikalike.
Mabomu hayo yalilindima maeneo mbalimbali ya mji ikiwemo eneo  maarufu la Makoroboi  kufuatia kuvunjwa kwa vibanda vya machinga jana asubuhi hali iliyowafanya wacharuke na kuanza mapambano na askari polisi na mgambo wa Jiji huku wakishinikiza wenzao walio kwenye maeneo halali nao waondolewe ili wote waikose makoroboi.

Katika sekeseke hilo wamachinga  zaidi ya 40 wamekamatwa kwa kukiuka sheria za mipango miji.

Hatua hiyo inafuatia maamuzi ya baraza la halimashauri ya Jiji la Mwanza kusafisha biashara “chafu” ya wamachinga kwenye maeneo ambayo hayaruhusiwi kisheria.
Vijana waandamanaji wakifunga barabara, ingawa kuna walakini je hawa nao ni machinga? Abdukadri Salim anasema kuwa vijana wanatumiwa kufanya vurugu na siyowamachinga. (MSIKILIZE KWA KUBOFYA PLAY)

Jeshi la polisi katika doria mtaa kwa mtaa.
Hapakukalika.
Hakuna biashara kila mtaa uligeuka kuwa mchungu.
Askari zimamoto washiriki zoezi la kuzima moto uliowashwa na wamachinga na kuhatarisha usalama wa msikiti wa Hindu wanaosali masinga singa. 
Eneo hili la kutoka barabara ya Lumumba linaloingia Makoroboi hadi kupitia msikiti wa Hindu (ukuta wa mahala panapo zimwa moto) na kuingia barabara ya Nyerere linatakiwa kuwa wazi bila kuwa na wafanyabiashara wanaotandaza bidhaa zao chini au kuegesha kunye kuta, na tukio la leo ni la zaidi ya mara mbili kutokea kwa wamachinga  kulikalia kwa nguvu.
Oparesheni ofisa wa zima moto, Sajenti meja Gadafi Masoud  amesema msikiti wa Hindu wanaosali masinga singa umenusurika kuchomwa moto na machinga hao baada ya magari makubwa mawili kikosi chake kuuzima moto uliowashwa na wamachinga kwa lengo la kuuteketeza msikiti huo ulio katika eneo waliloondolewa.(MSIKILIZE KWA KUBOFYA PLAY)

Mbali ya milindimo ya mabomu ili kudhibiti vyema vurugu hizo ilibidi jeshi la polisi mkoani hapa lifanye msako mtaa baada ya mtaa kuwasaka waanzisha fujo sanjari na kulinda usalamawa mali za wafanyabiashara kwani vurugu hizo zilizmbatana na uporaji.
Katika mitaa ya Makoroboi hata kwa wale wawamachinga walioruhusiwa kufanya biashara kutokana na kuwa katika maeneo sahihi ya ramani walishindwa kuendelea kutokana na vurugu hizo. 
Milindimo ya mabomu na moshi wake uliwapa wakati mgumu pia wanahabari.
Jeshi la polisi mkoani Mwanza lilitoa tahadhari ya watu kutosimama kwa makundi.
Mikakati ikifanyika kusuia maafa.
Hakika ni hasara kubwa kwa huduma na maduka ya biashara kufungwa kwa muda mwingi hali ambayo imewapa usumbufu mkubwa wateja kutoka katika mikoa ya jirani ya Mara, Shinyanga, Kagera, Simiyu na Geita waliohitaji bidhaa katika maduka ya jumla.
Kamanda wa polisi mkoani Mwanza Valentino Mlowola hakuweza kupatikana kwa kuwa yuko safari kikazi na msaidizi wake Christopher Fuime alidaiwa kuwa katika oparesheni hiyo huku baadhi ya askari ambao hawakutaka  kutajwa majina yao wakisema zaidi ya wamachinga 40 wamekamatwa  kuhusiana na vurugu hizo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.