ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 7, 2014

SHIRIKA LA TAIFA LA HIFADHI YA JAMII NSSF LATOA SEMINA KWA WACHIMBAJI WADOGO WAMADINI MWANZA.

Naibu waziri wa wizara ya Nishati na Madini nchini Steven Masele ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi akizindua Mpango maalum na kufungua Semina kwa wachimbaji wadogo wa madini iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano Victoria Palace Hotel Capripoint jijini Mwanza.
Meneja kiongozi wa Mfuko wa Hifadhi ya jamii NSSF mkoa wa Mwanza akitoa maelezo ya awali na kutambulisha wadau mbalimbali walio hudhuria Semina kwa wachimbaji wadogo wa madini iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano Victoria Palace Hotel Capripoint jijini Mwanza, ikiandaliwa na NSSF.
 "Mpango huu ni BIMA ambayo ukilipa utakusaidia katika huduma za matibabu wewe na familia yako lakini vilevile mwisho wa siku ukistaafu unachukuwa fedha kwaajili ya kuanza maisha mengine nje ya ajira, ikiwa ni sambamba na kukuwezesha katika suala la mikopo" Alisema Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la taifa la Hifadhi ya jamii NSSF Crescentius Magori.
Wadau wa NSSF wakinukuu pointi za msingi katika Semina ya wachimbaji wadogo wa madini iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano Victoria Palace Hotel Capripoint jijini Mwanza.
"Serikali imetumia zaidi ya shilingi milioni 250 kuwakusanya wachimbaji wadogo ili waweze kuwa na vyama vyao, wapate kutambuliwa ili wapate kusaidiwa," kisha akaongeza  Rais wa Shirikisho la wachimbaji madini Chama cha wachimbaji TZ (FEMATA) John Bina kwa kusema "Napenda kuwahakikishienikuwa kwa sasa wachimbaji wadogo tumejipanga, Ile dhana ambayo watanzania wengi wamekuwa nayo kuwa siye wachimbaji wadogo ni watu wa kutangatanga au wakuzurura haipo!"  
Mameneja wa NSSF Makao Makuu Dar es salaam, Viongozi wa NSSF mikoa ya Mara, Geita, Shinyanga, Singida, Kahama na Mwanza pamoja na viongozi wa FEMATA na vyama mbalimbali vya wachimbaji wadogo wamekutana hapa.
Wadau NSSF.
Katika hotuba yake ya Ufunguzi kwa niaba ya Serikali na wizara Naibu waziri wa wizara ya Nishati na Madini nchini Steven Masele ameishukuru NSSF kwa kukubali kufanya kazi na wachimbaji wadogo.
Wanahabari wakisaka picha zenye mvuto za kutazamika.
"Niliamini kuwa itatuchukuwa muda mrefu kusafiri kuweza kujenga na kutengeneza kitu ambacho kitatambulika kitaifa kitakuwa na heshima inayostahili na kitatoa mchango unaostahili na kitashawishi wachimbaji wengine kuona kwamba hii ni Fursa ambayo hakuna yeyote yule anayeweza kuiacha ipite pembeni. Sasa wacha niwapongeze NSSF kwa kuwa wajanja kati ya mifuko mingine yote ya jamii na kuamua kuliangalia kundi hili ambalo nguvu yake ya baadaye italiongoza taifa kuwa na matajiri wake wa ndani nikimaanisha wawekezaji wa ndani wenye nguvu Mabilionea"  alisema Masele.
Engo ya wadau washiriki wa semina kwa umakini.
Meza ya baadhi ya waratibu wa semina ya NSSF kwa wachimbaji wadogo wa madini iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano Victoria Palace Hotel Capripoint jijini Mwanza.
Kutoka meza kuu hadi kwa wadau washiriki wa semina ya NSSF kwa wachimbaji wadogo wa madini iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Serengeti, Victoria Palace Hotel Capripoint jijini Mwanza.
Naibu waziri Wizara ya Nishati na Madini Mhe. Steven Masele, akipata picha ya pamoja na Viongozi wa NSSF  pamoja na baadhi ya wanachama wa Chama cha wachimbaji wadogo wadogo wa madini (FEMATA). 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.