ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 23, 2014

GERMAIN KATANGA AHUKUMIWA JELA MIAKA 12

Kiongozi wa zamani wa wapiganaji waasi DRC Germain Katanga.
Mahakama ya kimataifa ya jinai ICC imemhukumu kiongozi wa zamanai wa wanamgambo waasi katika Jamuhuri ya kidemokrasi ya Kongo, Germain Katanga, kifungo cha miaka kumi na miwili jela baada ya kumpata na hatia ya uhalifu wa kivita.
Bwana Katanga alipatikana na hatia ya kuhusika katika mauaji ya mamia ya wanavijiji katikaeneo la Ituri Katanga mwezi Machi mwaka 2003.
Jimbo la Katanga ni jimbo lenye utajiri wa madini ya dhahabu kaskazini mashariki mwa nchi hiyo . Lakini kiongozi huyo wa waasi mwenye umri wa miaka thelathini na sita hakupatikana na hatia ya kuwatumikisha watoto vitani na makosa mengine ya ubakaji.
Chanzo BBC swahili.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.