ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 7, 2013

STARS YATINGA NUSU FAINALI CECAFA 2013

TIMU ya Kilimanjaro Stars imefanikiwa kusonga mbele hatua ya Nusu Fainali baada ya kuwatoa Mabingwa watetezi wa Kombe hilo Uganda kwa ushindi wa changamoto ya penalti 3-2 katika michuano ya kombe la Chalenji inayoendelea jijini Nairobi, shujaa akiwa kipa Ivo Mapunda .
Katika mchezo huo uliopigwa katika Uwanja wa Manispaa ya mji wa Mombasa,  Uganda ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza likifungwa na Daniel Sserunkuma katika dakika ya 16 akimalizia krosi ya Khamis Kiiza, bao ambalo halikudumu sana kabla ya Mrisho Ngassa kuisawazishia Stars kwa shuti kali  nje ya 18.
Baada ya bao hilo Stars walikuja juu na kufanikiwa kupata bao la pili likifungwa na Ngassa tena kwa mpira wa adhabu uliojaa wavuni katika dakika ya 39, matokeo ambayo yalidumu mpaka mwisho wa kipindi hicho cha kwanza.
Kipindi cha pili Stars inayofundishwa na kocha Kim Poulsen, raia wa Denmark, ilipata pigo katikati ya kipindi hicho baada ya kiungo wake Salum Abubakar 'Sure Boy' kutolewa kwa kadi nyekundu baada ya kucheza rafu, ambapo nafasi hiyo iliwapa nguvu Uganda kupata bao la kusawazisha kupitia Martin Mpuga matokeo ambayo yalibaki hivyo mpaka mwisho wa mchezo na kuzipeleka mpaka kwenye matuta.

Katika mikwaju ya penalti golikipa Ivo Mapunda alikuwa shujaa baada ya kucheza penalti mbili za Waganda ya beki  Khalis Alucho na  ile ya mwisho iliyopigwa na Sserunkuma ambayo ndiyo iliyoivusha stars.
Ifuatayo ni orodha ya waliopiga penalti katika mchezo huo.

Kili Stars                                                   Uganda
Erasto Nyoni (kakosa)                     Godfrey Walusimbi (kakosa)
Mbwana Samatta (kakosa)                Emanuel Okwi (kapata)
 Amri Kiemba (kapata)                      Khalis Alucho (kakosa)
Athuman Idd (kapata)                        Hamis Kiiza (kapata)
Kelvin Yondani (kapata)                    Sserunkuma (kakosa)

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.