ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 22, 2013

WASHINDI WA CLEAN HOUSE WAKABIDHIWA ZAWADI ZAO TOKA COLGATE PAMOLIVE

 Valarie Urio wa Dar es Salaam, anapokea jiko la Gesi cooker kutoka kwa Bi, Hytham Ahmed wa masoko Ltd kupitia promosheni iliyokuwa ikiendeshwa na Colgate Palmolive.
 Abeid Semira wa kutoka Mwanza anapokea zawadi yake kutoka kwa Bi, Hytham Ahmed wa Masoko Ltd. kupitia promosheni iliyokuwa ikiendeshwa na Colgate Palmolive.
Washindi wa Clean House wakabidhiwa zawadi zao toka Colgate Pamolive
Wakazi wa jijini Dar es salaam na mikoa ya Arusha, Mwanza na Mbeya waliokuwa wakinunua bidhaa za  Sta- Soft  na Axion (sabuni ya kuoshea vyombo) zinazosambazwa na Colgate Pamolive wamekabidhiwa zawadi zao kupitia promosheni iliyokuwa ikiendeshwa na Colgate Palmolive.

Kampuni ya Colgate Pamolive imekuwa ikiendesha promosheni  maalum ya CLEAN HOUSE kwa muda wa miezi miwili iliyokuwa na lengo la kuwafahamisha watanzania jinsi bidhaa zao za Sta- soft ambazo ni maalum kwa kufulia nguo na Axion maalum kwa usafi wa vyombo vya nyumbani. Bidhaa hizi ni maalum  kwa kufanya usafi kwa ufanisi mkubwa.

Akieezea bidhaa hizo Afisa Masoko wa Colgate Pamolive  Bw, Meshack Mdingi alisema “ Lengo la promosheni  hii ni kuwajulisha wateja wetu jinsi wanavyoweza kuepuka magonjwa ya ngozi kwa kufua nguo zao na Sta- soft inayotunza nguo zako na kuziweka laini  wakati wote na harufu nzuri na  kusafisha vyombo vya ndani.  Wateja wetu tunawashauri watumie  bidhaa yetu ya Axion inayofanya vyombo vibaki na mng’ao wake mzuri siku zote”

Walioibuka washindi kwenye promosheni ya Clean House ni wale wote walionunua bidhaa hizi kati ya September na Oktoba ambapo walichaguliwa kupitia droo maalum iliyofanyika wiki iliyopita maeneo ya Mwenge jijini Dar Es Salaam.

Baadhi ya walioibuka washindi  kupitia promosheni hiyo ni  Valeria Urio mkazi wa Dar Es Salaam, aliyejishindia Jiko la Gas cooker,  Abeid Semira mkaazi wa Mwanza aliyejishidia Jagi la Kuchemsha maji, Hassan Ibraim mkaazi wa Tanga kati ya wengine 50.

Bw, Mdingi alisema hadi kufikia mwisho wa promosheni  wameweza kuwaelimisha watu wengi kuhusiana na Usafi wa jamii, pia kurudisha faida wanazopata kwa jamii kwa kutoa zawadi ambapo jumla ya Majiko ya Gesi 3,Seti za Masufuria 8,  Seti za jagi za maji 8, pamoja na  mashine za umeme za kukausha mkate (Toaster) 8 za  kisasa kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na zawadi nyengine ndogo ndogo.

Kupitia bidhaa zetu bado tutaendelea kuwafikia wateja wengi kwa kufanya promosheni kama hizi huku tukitoa elimu kuhusiana na usafi kwa jamii na kutoa zawadi tofauti tofauti ili kuwafaidisha wale wote wanatumia bidhaa zetu za Colgate Pamolive, alimazia Bw, Mdingi

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.