ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 22, 2013

P-SQUARE WATINGA BONGO.

Wanamuziki wa kundi la P- Square Peter na Paul Okoye wakisalimiana na Mtangazaji wa kiruo cha Televisheni cha EATV, mapema baada ya kuwasili jana katika Uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Nyerer e jijini Dar es Salaam. Wasanii hao wameambatana na wasanii wengine 13 kutoka katika bendi yao. Tamasha hilo limeandaliwa naEast African Radio na EATV na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.
Mwanamuziki wa kundi la P- Square Peter Okoye akizungumza na waandishi wa habari, mapema baada ya kuwasili katika Uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Nyerer e jijini Dar es Salaam. Wasanii hao wameambatana na wasanii wengine 13 kutoka katika bendi yao.  Pamoja nao katika picha ni pacha wa msanii  huyo Paul Okoye ambao kwa pamoja wanaunda kundi la P - Square Tamasha hilo limeandaliwa na EATV na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania
Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu akizungumza na wasanii Peter na Paul Okoye punde baada ya kuwasili katika Uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Nyerer e jijini Dar es Salaam. Wasanii hao wameambatana na wasanii wengine 13 kutoka nchini Nigeria.
Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu  na Afisa Udhamini na Matukio wa kampuni hiyo  Ibrahim Kaude, wakiongozana na wasanii Peter na Paul Okoye punde baada ya kuwasili katika Uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Nyerer e jijini Dar es Salaam. Wasanii hao wameambatana na wasanii wengine 13 kutoka nchini Nigeria.
Mwanamuziki wa kundi la P - Square, Paul Okoye akiwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarake Nyerere, Tayari kwa ajili ya kutoa burudani kwa Watanzania, Msanii huyo aliambatana na Pacha wake Peter Okoye ambao kwa pamoja wanaunda kundi la P- Square. Wasanii hao wameambatana na wenzao 13 ambao watatoa burudani jumamosi ya tarehe 23 Novemba. Tamasha hilo limeandaliwa na East African Radio na EATV na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.