ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 7, 2013

MWANZA YASIMAMA KWA DAKIKA KADHAA.

Wakazi wa jiji la Mwanza leo majira ya saa 4 asubuhi waliwekwa njia panda na kujawa hofu kubwa kufuatia vikosi vya askari kanzu, FFU, askari polisi na zimamoto wakiwa na vifaa sambamba na magari yao walipolivamia jengo la Hotel Gold Crest na kuanza saka saka za kujiweka sawa huku wakiendeleza mapambano na jamaa ambao walijipanga mithili ya wahalifu.
Hali hiyo ilisababisha magari pikipiki kusimama kwa muda huku wananchi wakiingiwa hofu na woga, wengine wakikimbia na baadhi ya wafanyabiashara wakifunga maduka yao wakifananisha na lile la Westgate la jijini Nairobi nchini Kenya
Wateja wa kituo cha mafuta kilichopo karibu na hotel Gold Crest jengo ambalo ndiko zoezi lilikuwa likifanyika pamoja na wateja wa ofisi za PPF, duka la Vodacom Mwanza na Benki ya NMB zilizopo katika jengo hilo walikosa huduma kwa muda huku wengine wakitimka maeneo hayo kwa tahadhari wakidhani ni live.
Watu wakihaha nao polisi wakiweka ulinzi mkali eneo la tukio. 
Harakati zikiendelea eneo la tukio.
Polisi wakiwaweka chini ya ulinzi 'wahalifu bandia' katika zoezi lililozua taharuki kwa kwakazi wa jiji laMwanza.
Hata hivyo mpaka zoezi hilo linamalizika hakuna mwananchi aliyeweza kubaini kuwa tukio hilo lilikuwa ni la uigizaji, kila mmoja alikuwa akisimulia kivyake sekeseke zima, lakini mapango mzima ulikuwa ni kuvinoa vikosi vya polisi na Zimamoto juu ya kukabiliana na uhalifu kwenye majengo makubwa ya huduma mbalimbali. Ama hakika zoezi lilifanikiwa.

Pig up Jeshi la polisi mkoa wa Mwanza.

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. kaka weka maelezo basi ili tujue ni nini kilitokea

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.