ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 14, 2013

MH. LOWASSA AKUTANA NA WANAFUNZI WA VYUO VYA ELIMU YA JUU MKOANI TABORA NA KUTEMBELEA CHAMA CHA WAENDESHA BODABODA

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa (katikati) akiongozana na baadhi ya Viongozi wa Chama cha Mapinduzi Mkoani Tabora,wakati alipokuwa akiwasili kwenye Ofisi za CCM Wilaya ya Tabora Mjini,mchana wa leo Septemba 13,2013.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akisalimiana na baadhi ya viongozi wa CCM Wilaya ya Tabora waliofika kumlaki alipokuwa akiwasili Mkoani Tabora mchana wa leo Septemba 13,2013.
Msafara wa Pikipiki (maarufu kama Boda Boda) Mkoani Tabora ukiwa barabarani wakati wa kumpokea Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa alipokuwa akiwasili Mkoani Tabora leo,ambapo alitembelea Ofisi za Chama cha Waendesha Pikipiki (Bodaboda) Mkoani Tabora.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akisalimiana na baadhi ya wanachama wa Chama cha Waendesha Pikipiki (Bodaboda) Mkoani Tabora wakati alipokitembelea Chama hicho jioni ya leo Septemba 13,2013.Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama hicho,Waziri Kipusi.
Mwenyekiti wa Chama Waendesha Pikipiki (Bodaboda) Mkoani Tabora,Waziri Kipusi (kushoto) akisoma taarifa fupi mbele ya Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa juu ya mwenyendo wa Chama hicho pamoja na malengo yake.ambapo Mh. Lowassa ameahidi kuwapatia pikipiki tatu,ikiwa ni sehemu ya mchango wake kwenye Chama hicho.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akizungumza machache kwenye mkutano wake ya Waendesha Boda Boda wa Mkoa wa Tabora.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akizungumza jambo na Watoto waliojitokeza kumsalimia wakati alipokuwa akiwasili Mkoani Tabora leo,Septemba 13,2013.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akifurahia jambo na Watoto Chipukizi waliokuwepo nje ya Ofisi za CCM Wilaya ya Tabora Mjini.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa (mwenye kipaza sauti) akisisitiza jambo wakati akizungumza na Wanafunzi wa Vyo mbali mbali Mkoani Tabora,waliokuwa wamefurika kwa wingi kwenye Ukumbi wa Chuo cha Utumishi,Mkoani Tabora leo Septemba 13,2013.
Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Tabora Mjini,Seif Gulamali akizungumza machache mbele ya Wanafunzi wa Vyuo mbali mbali Mkoani Tabora leo.
Mbunge wa Jimbo la Urambo,Mh. Athuman Kapuya akijibu moja ya Maswali yaliyokuwa yakiulizwa na Wanafunzi hao wa Vyuo mbali mbali Mkoani Tabora waliokuwa wamefurika kwa wingi ndani ya Ukumbi wa Chuo cha Utumishi Mkoani humo,kumsikiliza Mh. Lowassa.
Baadhi ya wanafunzi hao kutoka Vyuo mbali mbali Mkoani Tabora,wakiuliza maswali.
Baadhi ya wanafunzi hao kutoka Vyuo mbali mbali Mkoani Tabora,wakiuliza maswali.
Baadhi ya wanafunzi hao kutoka Vyuo mbali mbali Mkoani Tabora,wakiuliza maswali.
Wanafunzi kutoka Vyuo mbali mbali Mkoani Tabora kusanyikoni.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.