ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 14, 2013

AIRTEL YAWAOMBA WATANZANIA KUWAOKOA WAWAKILISHI WA TZ BBA


·        Wateja wa Airtel Lipieni DSTV kwa Airtel Money mambo mazuri yaja

Watanzani wametakiwa kuwapigia kura nyingi kadri wawezavyo, wawakilishi wao katika shindano la Big Brother Africa ‘The Chase’ linaloendelea nchini Afrika Kusini ili kuhakikisha wanaendelea kubaki ‘mjengoni’ wakipeperusha bendera ya taifa.

Wito huo, umetolewa na Meneja Uhusiano wa Kampuni ya simu ya Airtel Tanzania, nayodhamini shindano hilo,Jackson Mmbando, huku akiwataja wawakilishi hao wa Tanzania kuwa ni Feza Kessy  na Ammy Nando. 

Mmbandoalisema kuwa, ili kuendelea kumbakisha Feza katika kinyang’anyiro cha BBA ‘The Chase,’ Watanzania wanapaswa kutuma ujumbe wenye jina ‘FEZA’ kwenda namba 15456, ili kumuokoa mshiriki huyo aliyeingia mara mbili kikaangoni, tofauti na Nando(22), ambaye anafanya vizuri.

“Watanzania tuna kila sababu za kuwapigia kura wawakilishi wetu, ili waweze kuwakilisha vema na kipaumbele zaidi kiwe kwa kumpigia Feza kwa kuandika jina lake kwa herufi kubwa “FEZA” kisha kwenda kwa namba 15456,” alisema Mmbando.

Mshindi wa mwaka huu, atajinyakulia kitita cha Dola za 300,000 za Marekani.Tangu shindano hilo lianze ni Mtanzania Richard, ndiye pekee aliyewahi kushinda shindano hilo.

Mashindanohayo yanayofanyika kwa mara ya nane, yanashirikisha washiriki 24 kutoka nchi 14za Afrika na watakaa ndani ya nyumba hiyo kwa siku 90, ambako kusalia kwao mjengoni kunategemea kura za watazamaji wa shindano hilo.

Katikahatua nyingine, Mmbando aliwataka Watanzania kuendelea kulipia huduma zao zaDSTV kupitia Airtel money, kwani kuna kuna kitu cha ziada kinakuja kwa ajili yao.

“Airtel ili kuleta burudani zaidi kwa wale wanaolipia huduma na vifurushi vya kila mwezi vya DSTV kupitia huduma ya Airtel Money kuna mambo mazuri yenye kuvutia yanakuja yatakayowafanya waendeleee kutosheka zaidi kupitia huduma zetu zote” alimaliza kwa kusema bw, Mmbando.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.