ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 9, 2013

RAIS JAKAYA KIKWETE AMTEMBELEA KIBANDA SOUTH AFRIKA.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali mhariri Mtendaji wa Habari Corporation Absalom Kibanda aliyelazwa katika hospitali ya Mill Park iliyopo mji wa Johannesburg, Afrika Kusini jana Ijumaa. Kulia ni Katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana. Bwana Kibanda alipelekwa Afrika Kusini kwa matibabu zaidi baada ya kujeruhiwa vibaya na watu wasiojulikana juzi usiku. Rais Kikwete yupo Afrika Kusini kuhudhuria Mkutano wa Viongozi wa Vyama vilivyokuwa mstari wa Mbele katika mapambano dhidi ya Ukoloni na ubaguzi wa Rangi. Mkutano huo umeandaliwa na Chama cha African National Congress (ANC). Picha zote na Freddy Maro.


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali mhariri Mtendaji wa Habari Corporation Absalom Kibanda aliyelazwa katika hospitali ya Mill Park iliyopo mji wa Johannesburg, Afrika Kusini jana jioni. Kulia ni Katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana. Bwana Kibanda alipelekwa Afrika Kusini kwa matibabu zaidi baada ya kujeruhiwa vibaya na watu wasiojulikana juzi usiku. Rais Kikwete yupo Afrika Kusini kuhudhuria Mkutano wa Viongozi wa Vyama vilivyokuwa mstari wa Mbele katika mapambano dhidi ya Ukoloni na ubaguzi wa Rangi. Mkutano huo umeandaliwa na Chama cha African National Congress (ANC).

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.