ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 13, 2012

PRIMETIMES PROMOTIONS WAWAPONGEZA WADHAMINI SERENGETI FIESTA 2012

Mkurugenzi wa Clouds Media Group Joseph Kusaga akitoa shukurani kwa Wadhamini wakuu waliofanikisha Serengeti Fiesta 2012 kufanyika na kumalizika kwa amani kwa mikoa takribani 12 nchini Tanzania ile hali tamasha hilo likiacha alama ya maendeleo na chembe za changamoto ya ukuzaji uchumi kwa wananchi wa mikoa iliyo kuwa kwenye ratiba. 

Mkurugenzi wa Clouds Media Group Joseph Kusaga akitoa Cheti cha Ushiriki bora kwa wadhamini wa mafuta vyombo vya barabarani GAPCO walioshiriki vyema Tamasha la Serengeti Fiesta 2012. 

Mkurugenzi wa Clouds Media Group Joseph Kusaga akitoa Cheti cha Ushiriki Bora kwa wadhamini wakuu Kampuni ya bia SBL kupitia kinywaji mahsusi Tamasha la Serengeti Fiesta 2012, Serengeti Premium Lager walioshiriki vyema kufanikisha mpango mzima mwanzo mwisho. 

Kisha zikafuata shukurani za dhati kutoka kwa Mdhamini mkuu zilizotolewa na Mkurugenzi wa Masoko bia ya Serengeti Ephaim Mafuru.

Msanii mahiri mwenye mbwembwe za kila aina Juma Nature akimwimbia Mtangazaji wa kipindi cha Jahazi Wasiwasi Mwabulambo 'aaaah ... naye alicheza siutani' 

Top in Dar, You can call him TID naye alipata fursa kutoa shukurani zake katika usiku huo maalum wa marafiki kukutana ndani ya Escape Two.

Kwa upande wa msanii wa muziki wa kizazi kipya Shettah amesema kuwa ujio wa tamasha hilo mwaka huu 2012 umetumika kuijenga sanaa yake sambamba na kumweka karibu na mashabiki wake ana uhakika kupata mialiko mingi ya kutosha kwani amekwisha jitangaza vya kutosha naye amejipanga kufanya show levo za kimataifa. 

Mwana FA kwa upande wake amesema hii ni miaka yake ya kusherehekea mafanikio kwa sanaa yake kushika hatamu akimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumtunuku karama ya ubunifu wa mashairi, nyimbo za kueleweka pamoja na umiliki bora wa jukwaa na hadhira.

Tajiri wa Sauti aka Rich Mavoko na shukurani zake ndani ya Part Maalum la Shukurani lililoandaliwa na Primetimes Promotion kuwapongeza wadhamini wa Serengeti Fiesta 2012 nakufanyika Club Escape Two jijini Dar es salaam.

Hip hop thing'

Mchekeshaji maarufu nchini Tanzania toka kundi la Vuvuzela Entertainment,  Bukuku (katikati) akiwa na wadau.

The Crew.

Watu waliunyuka.....

Wawo....

Men....

Ni Dr. Isaack, Fid Q na mie.

Ze Crew...

Shine....
  
Producer wa Clouds Tv Mr. Mebb.

Dj Mayanga on the one and two.

Fun moment ni Madee, Chege, Morgan na Wasiwasi.
Good.

Wanyama....

Inshort kila kitu kili shine usiku wa jana...
Shukurani kwa Primetimes Promotion kwa kutukutanisha,
Serengeti Premium Lager, GAPCO, PEPSI na Precission Air kwa udhamini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.