ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, February 7, 2012

SHEREHE ZA CCM KILA MDAU ANASEMA LAKE

Ze Videoz'Mambo matamu live.
Basiz' zilizopaki viwanja vya Furahisha nje ya CCM kirumba.
@Kwa tunaoijua vizuri Mwanza, tumefurahi kuona idadi kubwa ya watu waliojazana uwanja wa Kirumba jana wakiwa ni wana vijiji waliosombwa kwa malori, mabasi, na usafiri mwingine kuja Mwanza kucheza ngoma za sungusungu, kugawiwa t-shirt, kanaga na kofia, kula wali nyama, kuona jiji la Mwanza, kuuonekana kwenye luniga, na kisha kupatiwa shilingi 2000 kila mmoja. Safi sana! Wengi walitoka wilaya za vijijini; Magu, Kwimba, Misungwi, na wachache toka wilaya zenye miji kama Sengerema na Geita. Wajanja wenyewe wa Mwanza mjini hawakujisumbua. Na bila kusomba watu toka vijijini - yaani wale maskini wasioweza kupata hata sh 1000 kwa mwezi, CCM itapata wapi watu kwenye mikutano yao? Mchezo wa kizamaaaaaaaani. Kama mnabisha, subiri kilio cha CCM mkoa wa Mwanza uchaguzi mkuu 2015. Hivi hamuwajui wasukuma? Wakisema "twalemaga" ndo "twalemaga" kweli! Unaweza kucheka nao, ukawapa pesa wakachukua, ukawapo wali wakala, na kibano bado unapata. Kamuulize .....!
Nyomiz' ndani ya CCM Kirumba
@Wengine wengi tu leo wamerudishwa makwao, kogongo ferry kulikuwa na coaster moja, bus la mohamed trans na hiance nguo zile zile za jana wanatia huruma wako hoi midomo mikavu!
Fusoz' uwanja wa Furahisha nje ya dimba la CCM Kirumba.
@Mh hivi kweli watu mko serious au ni chuki tu. Nani kasema Watanzania hawana uhuru wa kusafiri kokote nchini? Mnashangaa nini watu kuchukuliwa na mabasi kukutana Kirumba CCM? Si ndiko ilikuwa RV yao kwa ajili ya maadhimisho? Mlitaka wakanyage kwa mguu kutoka Kisesa, Kigongo, Ukiriguru na kwingineko kuja mjini Mwanza? Acheni hizo!

@Watu wanazidi miminika uwanjani hapa, ukweli ni watu ni wengi kutokana kuletwa na Mabasi Makubwa. Uwanja wa ndani ile pich ya kuchezea kandanda imefurika vikundi takribani 50 hivi vya ngoma wakiongozwa na TOT.

Mbonjiz'katikati ya sherehe.
@Jamani kila raia ana haki ya kusema chochote ilimradi asivunje Sheria za Nchi. Tatizo ni kwamba tunapenda kusikia habari za aina fulani tu. Wacha watu wajimwaage wawe wamenunuliwa ama lah kila mmoja anasaka ugali wa familia. Wenye mabasi nao wanatafuta ugali kama Kirumba ndiko kunalipa hata mimi ningekuwa dereva ama utingo ningepeleka gari huko.

@Nimeingia Mwanza leo asubuhi, kitu kilicho nishangaza ni kuonaMabasi yalikuwa yakizunguka mji mzima leo yakibeba watu kuelekea kilumba! Inashangaza kuona kwanini ccm wanatumia nguvu kubwa hivyo kukusanya watu? Hii inaashiria nini?
Paul Masatu,

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. SENGO,
    ASANTE KWA TAARIFA ZA SHEREHE YA MIAKA 35 YA CCM. NAWAPA POLE SANA WANAODHANI CCM IMEKUFA. UKIONA SIMBA AMELOA USIZANANI NYANI ITAKULA KWAKO. WALE WABUNGE WA UPEPO WASUBURI ITAKAVYO KULA KWAO

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.