ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, February 19, 2012

BOBBY AUAGA MWILI WA WHITNEY CHINI YA ULINZI MKALI AHUDHIRIA MISA KWA DAKIKA 15 TU KISHA ATOWEKA KWENYE TUKIO

Wakati mwili wa mwanamuziki Whitney Houston ukiwa ndani ya kanisa la Newark's New Hope Baptist siku ya jumamosi. Kulikuwa na mtu mmoja tu ambaye macho ya wengi yalikuwa yameelekezwa kwake kimtindo tena kwa saaaana yakimjadili kwa namna tofauti kuona naye ana hisia zipi juu ya msiba huo, si mwingine bali ni mume wa zamani wa Whitney, Bobby Brown.

Shuhuda wa gazeti la Us Weekly aliyekuwa karibu na tukio amepenyeza habari kuwa "Licha ya taarifa za awali kwa mume huyo wa zamani kuchimbwa mkwara kwa kupigwa marufuku kuhudhuria misa ya mazishi, atimaye aliruhusiwa kutinga ndani ya kanisa kutoa heshima zake za mwisho na kutakiwa kuondoka mara moja. Akiwa na macho mekundu alikwenda kwenye jeneza na kulibusu kisha akasepa zake. Alikuwa pale kwa dakika 15 tu."

"Mie na mtoto wangu tulialikwa kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa mke wangu Whitney Houston. Tulikaa chini ya uangalizi wa wanausalama muda mchache tukatenganishwa sehemu tatu tofauti. Nilishindwa kuelewa kwanini walinzi walitufanyia hivyo huku wakitoa amri hakuna ruksa ya kusogea wakinizuia mie kumsogelea binti yangu Bobbi Kristina. In light of the events, I gave a kiss to the casket of my ex-wife and departed as I refused to create a scene. I doubt Whitney would have wanted this to occur. I will continue to pay my respects to my ex-wife the best way I know how." Alisema Bobby.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.