ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, January 25, 2012

IDHAA YA REDIO JAPANI KUSIKIKA LIVE FEBRUARI MOSI 2012 KUPITIA TBC FM

Kuanzia Feb mosi mwaka huu, matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya Redio Japani yatasikika moja kwa moja kupitia TBC FM Dar es salaam baada ya mkataba rasmi kutiwa saini mwishoni mwa wiki iliyopita Jumamosi tarehe 21/1...jijini Dar es salaam. Ilikuwa hafla iliyohudhuriwa na Mkurugenzi mtendaji wa TBC Bw.Clement Mshana aliyetia saini kwa niaba ya TBC na Mwakilishi wa NHK World Bi Yuko Asano akiwa na ujumbe wake wa watu watano kutoka Japani. Waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na balozi wa Japani Nchini Tanzania Mh. Okada , Mkurugenzi wa habari maelezo Bw. Raphael Hokororo aliyesoma hotuba kwa niaba ya waziri wa Habari, utamaduni na Michezo mh. Emannuel Nchimbi, na wadau wengine wakiwemo wasikilizaji wa radio japani kutoka katika nchi za Kenya, Uganda na wa nyumbani Tanzania. Mwingine ni makamu wa Mwenyekiti wa Bodi ya TBC na wafanyakazi wa TBC waliotoa support sana.. tafadhali fuatilia habari hizi kwa njia ya picha.

Shughli watu...

Shughuli haikuwa ndogo...mbali na viongozi Meza kuu.. mkuu wa TBC FM Bw. Othmn Iddi aliongea katika hafla hiyo,

Ilifana...

Mmoja wa wasikilizaji wa Redio Japani Generoza Ndunguru (Picha ya chini)mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma, akiongea katika hafla hiyo...

Picha ya pamoja.
CHANZO MIRINDIMO

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.