ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, October 31, 2011

5/11/2011 NI AROBAINI YA MZEE WETU MAREHEMU GEORGE MHANDO

Marehemu George Mhando.
Salaam aleykum ndugu zangu nyote, poleni na majukumu, aksanteni kwa kushiriki kikamilifu wakati wa msiba wa baba yetu mpendwa uliotokea tarehe 1/10/2011 kisha tukampumzisha kwa amani mpendwa wetu.

Arobaini itafanyika jumamosi ya tarehe 5/11/2011 kuanzia saa kumi jioni kuamkia jumapili tutakuwa na mkesha wa mila ya kushukuru Kibondei kutokana na umri wake kufikia miaka 90. Arobaini itafanyika Muheza kijiji cha Enzi njia ya kwenda Pangani kilometa 3.
Karibuni tushiriki

Ndimi mtoto wa Marehemu
Omary G. Mhando.
Muheza, Tanga.

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. ooh Mungu azidi kutupa nguvu kwani baba alikua mfano mzuri sana kwa Taifa hili.

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.