1. The borders are entirely free (hakuna cha afisa uhamiaji, hakuna cha polisi, hakuna cha passipoti, hakuna chochote). Labda vibao vinavyokuonyesha ..sasa unaingia mfano Uholanzi, au Denmark au Ujerumani.
2. Nishati: Ninaposikia sakata la umeme nchini kwetu, najiuliza maswali mengi? Mbona huku ulaya wanazima mitambo yao ya kufufua umeme na kuwekeza katika nishati endelevu ya upepo na umeme wa jua?
Kwa nini TANESCO au SERIKALI (wizara husika) isiwekeze katika umeme kama huu wa jua au upepo. Nikiangalia tuna bahari na coastline ndefu sana. Je tungeliwekeza katika umeme wa upepo, tusingepata umeme mwingi? Mbona hawa wameweza jamani? Nakuletea picha hizi chache uone huku wanavyoweza...
Sisi mara Richmondi, mara Songeshaz' mara nini,... hatutafika popote. Jua tunalo la kutosha, upepo tunao wakutosha.
3. Miundo mbinu: Natoka mkoa wa Kagera na usafiri wa maji tulionao umebaki meli moja tu ya Mv Victoria, ambayo imesafiri katika ziwa hili kwa zaidi ya miaka 40? Na juzi nimetembelea mji wa Panerbug ilipotengenezwa meli ya MV Liemba iliyoko katika mji wa Kigoma, nikakuta sasa wao wameisha fikia uwezo wa kutengeneza meli kubwa sana duniani. Nakuletea picha hapa Angalia meli hiyo ukubwa wake.
4. Miundo mbinu, usiseme. Na kwa upande wa barabara, nilikuwa najiuliza ili kasumba na tararatibu za BOMOA BOMOA, nimejiuliza nikasema kuwa, kama watu tayari wanaishi katika mazingira, na sasa unataka kutengeneza barabara, kwa nini barabara hiyo isipite katika maeneo ambayo hayana makazi? si lazima kusumbua utarataibu na makazi ya watu. Barabara kuu inarahisisha uchukuzi.. si miji hata ikibaki pembeni, inaweza kuunganika na barabara kuu kuliko, kubomoa nyumba za watu, n.k?
Samahani kaka kwani picha ni nyingi kidogo na labda hauna bandwidth ya kutosha.
Wako,
Joseph Sekiku
Ujerumani
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.