Utashi wa viongozi, uwezo duni wa wasimamizi, viongozi kujali maslahi binafsi na kuweka kando maslahi ya Umma ni moja kati ya mambo yaliyojitokeza na kutiliwa mkazo leo hii kwenye kipindi cha 'Tuongee Asubuhi' kupitia Star Tv ambapo mada kuu ilikuwa ni kuijadili Hotuba ya Bajeti ya Serikali ya Mwaka 2011/2012 iliyotolewa jumatano (trh 8 juni) na waziri wa fedha na Uchumi Bw. mustapha Mkulo.
Nimefurahishwa na sms nilizokutana nazo kwenye simu yangu moja ikisema 'Pombe, sigara na mvinyo hata vikipanda kwa asilimia ngapi, kiwango chochote mimi na wanywaji wenzangu tutaendelea kunywa tu hadi kieleweke kwani wanywaji hawana bajeti'
TAKWIMU ZA BAJETI:
Mfumuko wa bei hadi April 2011......8.6%
Pato la Mwananchi hadi 2010..........sh.770,463
Akiba ya Dola hadi desemba 2010.....$milioni 3,948
Ukuaji wa uchumi mwaka 2010.........7%
Riba katika mabenki mwaka 2009......13.4%
Shilingi kuporomoka mwaka 2009......8.5%
Thamani ya Shilingi kwa dola ...........$1=1432
Uuzaji biashara nje umekuwa 2009....24%
Akaunti katika mabenki...................4,241,610
Matawi ya benki nchini yamefikia.......475
ATM nchi nzima zimefikia.................966
Mapato ya ndani (2010)yameongezeka..8.7%
Deni la Taifa limekuwa hadi..............$millioni 11,380
Nguvu kazi ya Taifa 22,661,280.........52.7%
Wenye ajira milioni 8......................35.3%
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.