ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 1, 2011

MKALI NANI KATI BONGO FLEVA V/S MWANZA STAR KUJULIKANA KESHO CCM KIRUMBA.

Kutoka kushoto H.baba, Inspector Haroon, Kabago, Jebby, Ben Kinyaiya, Suma G. na Mansulee.

Ule mtanange wa kukata na shoka unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka kanda ya ziwa baina ya timu ya Bongo Fleva na Watangazaji & Madj wa jiji la Mwanza aka 'Mwanza stars' ndiyo hivyoo umebakiza saa kadhaa upate kuchukuwa nafasi, nazungumzia kesho jumamosi katika dimba la CCM kirumba.

Tayari baadhi ya wachezaji wa timu ya Bongo Fleva wamekwisha wasili jijini Mwanza kwaajili ya mpambano huo wakishiriki hatua kadhaa za matayarisho ya kipute hicho huku wengine wakitaraji kutua usiku wa leo na Precision air Pichani kutoka kushoto ni H.Baba (jembe la Bongo fleva) Suma (Bf) Philbert Kabago (kapten wa Mwanza stars) Omari (mratibu wa pambano) na G.Sengo (Mzs')baada ya mahojiano Radio Passion mchana wa leo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.