Wagombea wa kiti cha urais na ubunge nchini Uganda, wanatarajiwa kukamilisha kampeini zao hii leo tayari kwa uchaguzi mkuu utakaofanmyika siku ya Ijumaa.Rais Yoweri Museveni, ambaye anawania muhula wa nne kama rais wa Uganda, kupitia chama tawala cha national Resistance Movement, NRM, anatarajiwa kufanya kikao na waandishi wa habari leo asubuhi, kabla ya kukamilisha kampeini yake na mkutano wa hadhara mjini Kampala.
Nae Mpinzani mkuu wa rais Museveni, Kizza Besigye (pichani kushoto) anayewania kiti hicho kupitia chama cha Forum for Democratic Change, FDC, naye atakuwa na mkutano katika chuo kikuu kimoja mjini Kampala.
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini humo, Badru Kiggundu, ametoa wito kwa viongozi wa vyama vyote vya kisiasa nchini humo, kuvunja makundi yote ya wapiganaji ambayo yaliundwa kwa dhamira ya kulinda masanduki ya kupigia kura.
Blogu hii ya jamii inawatakia Uchaguzi Mwema wa Amani wananchi wa Uganda.
RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA
-
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe.
Mwanaidi Ali Khamis akigawa iftar kwa mmoja ya mtoto anayelelewa katka
Makao ...
Awaachie wenzake sasa hee! Africa bwana.
ReplyDelete