
Maadhimisho ya mwaka huu yamegubikwa na utata unaondelea juu ya mipango ya kujenga kituo ca kiislam karibu na viwanja vya mashambulizi hayo mjini New York, na tishio, ambalo sasa limesitishwa, la kasisi wa kanisa moja ndogo katika jimbo la Florida kutaka kuchoma moto nakala za kitabu cha Koran.


Bw Obama alisema kuchoma maandishi ya kidini ni kinyume na maadili mema ambayo ndiyo msingi wa Marekani.
Kasisi anayetaka kutekeleza kitendo hicho, Terry Jones, amesema amesitisha mpango wake wa kuchoma Koran wakati wa maadhimisho ya mashambulizi ya Septemba kumi na moja , lakini anataka kukutana na Imam anayesimamia mpango wa kutaka kujenga kituo cha kiislam karibu na eneo la jengo lililoangushwa katika mashambulizi hayo la World Trade centre mjini New York.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.