ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, July 22, 2010

MKUU WA WAILAYA YA NYAMAGANA ATUTOKA

CLEORHAS ANGELLO RUGALABAMU.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda ametoa salamu za rambi rambi na pole kutokana na kifo cha Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, mkoani Mwanza, Bw. Cleophas Angello Rugalabamu kilichotokea mapema jana nchini India ambako alikuwa anatibiwa.

Bw. Rugalabamu (64) alilazwa katika Hospitali ya Appolo mjini Chennai tangu Juni 20 mwaka huu na alifariki dunia leo alfajiri.

Mipango inafanywa ya kurejesha maiti yake nchini kwa ajili ya mazishi. Katika salamu zake alizozituma kwa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Yohana Balele, ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Pinda alisema kifo cha Bw. Rugalabamu kimeleta majonzi makubwa.

“Alikuwa kiongozi hodari na muaminifu. Kwa niaba ya Serikali na kwa niaba yangu mimi mwenyewe binafsi, natoa rambirambi na pole kwa familia ya marehemu, ndugu jamaa na marafiki kutokana na msiba huo.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi,” Waziri Mkuu alisema katika salamu hizo.

Imetolewa na: Ofisi ya Waziri Mkuu
S.L.P. 3021
DAR ES SALAAM
Jumatano Julai 21, 2010

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.