ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, October 6, 2022

BODABODA APIGWA PESA NA MGANGA AKISAKA MAFANIKIO

 


Mhudumu wa boda boda kutoka Loitoktok, Kaunti ya Kajiado amemshtaki mganaga wa kienyeji kwa kumtapeli KSh 543,200 (Zaidi ya milioni 9 za Kitanzania). 

 Mhudumu huyo, Dickson Murigi, alimwambia hakimu mkuu wa mahakama ya Loitoktok Judicaster Nthuku kwamba Mwaima Mbwana Kiungumi, aliahidi kuzidisha pesa zake na kumfanya awe milionea. 

Murigi alisema, mnamo Septemba 3, 2021, mkewe Jane Wambui, alimfahamisha kulikuwepo na mganga mashuhuri Nairobi, aliyetaka kumkaribisha nyumbani kwao.

Mganga huyo alifika nyumbani kwao baadaye siku hiyo, baada ya mumewe Wambui kumtumia nauli ya KSh 2,000 

 Murigi aliaambia mahakama kuwa Mwaima ambaye ni mganga aliitisha KSh 12,000 na kumpa pesa hizo. Mlalamishi alisema mganga huyo alianza kufanya mazingaombwe, na kuona kitita cha shilingi milioni 300. 

Hata hivyo, wakati huo huo, mganga huyo aiisema pesa hizo zilimea mabawa na kupuruka kwa njia tatanishi. 

Baada ya jaribio la kwanza kufeli, Murigi alimkabidhi KSh 152,000, ambayo alikuwa amezifunga kwa suruali yake ya ndani na kuweka mvunguni mwa kitanda. 

Murigi alisema hatimaye Mwaima alimpeleka kwenye pango moja Mombasa, na kusikia sauti iliyosema anafaa kuongeza KSh 400,000 zingine. Murigi alisema aliuza mali yake na wakati alipoishiwa na pesa za kumtumia mganga huyo, alitoweka na kukoma kupokea simu zake. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.