ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 16, 2016

TCRA YAVIFUNGIA VITUO 21 VYA RADIO NA 6 VYA TELEVISION KWA MUDA WA MIEZI 3 KUANZIA JUMATATU TAREHE 18

TCRA yavifungia vituo 21 vya Radio na 6 vya Television kwa muda wa miezi 3 kuanzia Jumatatu tarehe 18.
NI VITUO VIFUATAVYO>-
1. Sibuka fm 2. Breez fm 3. Country fm 4. Ebony fm 5. Hot fm 6. Impact fm 7. Iringa manicipal Tv 8. Kiss fm 9. Kitulo fm 10. Kifimbo fm 11. Mbeya city municipal Tv 12. Radio 5 13. Radio free Afrika 14. Musa Television network 15. Pride fm radio 16. Radio huruma 17. Radio uhuru 18. Star Tv 19. Rock fm radio 20. Standard fm radio 21. Sumbawanga municipal Tv 22. Tanga City Tv 23. Top radio fm limited 24. Ulanga fm

Vituo hivi vimefungiwa kutoa huduma kwa muda wa miezi 3 kwa sababu ya kutolipa ada/kodi
Mwezi July 2015 ilitolewa taarifa kwa umma na TCRA kwamba baadhi ya radio na Televisheni zipatazo 40 zinadaiwa ada na tozo mbalimbali.
Septemba 28 vyombo hivyo vikapewa onyo la mwisho kwamba hadi Tar 31 dec wawe wamelipa ada zao ambapo wengine walilipa Jan 4. Wengine wakakausha.
Kwa mujibu wa sheria unapokua hujalipa kodi TCRA wanakuchukulia kuwa wewe hu exist.
TCRA wanasema hata miezi 3 ya adhabu ikiisha na bado haujalipa further actions kama kunyang'anywa leseni kunaweza kutokea.
Ni vituo 11 tu kati ya vituo vilivyokuwa vinadawa na mamlaka vilitii.
Sasa basi TCRA wanasema kuanzia Jumatatu tar 18, Radio 21 na TV 6, vituo hivi havitatakiwa kuwa hewani kufanya kazi kutokana na tamko la mkurugenzi wa TCRA

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.