ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, November 24, 2025

UBUNIFU WA KIPEKEE KISIWA CHA SAANANE WAIBUKA A TUZO

Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kisiwa cha Saanane, Kamishna Msadizi wa Uhifadhi Dkt. Tutindaga George, akipokea Tuzo ya Ubunifu wa Mazao ya Utalii, jijini Dar es Salaam.

Ubunifu wake wa kipekee umevuka mipaka ya kawaida na sasa umetambuliwa kitaifa!

 
Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi na Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kisiwa cha Saanane jijini Mwanza, Dkt. Tutindaga George, ametwaa Tuzo Maalum ya Ubunifu wa Mazao ya Utalii kama sehemu ya Top 100 Executives List Awards 2025.

Katika hafla ya heshima iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Novemba 20, 2025, Dkt. Tutindaga alitangazwa rasmi kuwa  
"Chief Innovation / Head of Product Design and Innovation of the Year."

Mazao ya Utalii Yaliyompa Tuzo
Kupitia kazi yake katika Hifadhi ya Saanane, Dkt. Tutindaga amebuni na kuboresha bidhaa kadhaa za kipekee za utalii, zikiwemo:  
• Boat Safari katika Ziwa Victoria
• Rock Hiking
• Maeneo ya mapumziko ya kisasa (picnic sites) 
• Michezo ya majini
• Kutazama machweo ya jua
• Uboreshaji wa malazi ya kitalii
Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kisiwa cha Saanane, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Dkt. Tutindaga George, akionesha Tuzo yake ya Ubunifu wa Mazao ya Utalii.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Dkt. Tutindaga aliwashukuru wote waliomuunga mkono na kutoa mwito kwa Watanzania kutembelea vivutio vyetu vya asili:

“Nashukuru sana kupata nafasi hii. Kama Mhifadhi, naendelea kuwakaribisha kutembelea Hifadhi ya Taifa Kisiwa cha Saanane.”

 Aliongeza kwa kumshukuru Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA, Musa Kuji, kwa kuendeleza mazingira wezeshi kwa wanawake katika uongozi na ubunifu:

“Tuzo hii si yangu peke yangu, ni heshima kwa TANAPA nzima, ushahidi kuwa ubunifu unazaa matokeo.”

Hifadhi zetu ni hazina ya Taifa
Kila unapozitembelea, unachangia uhifadhi, uchumi na maendeleo ya jamii.  

 


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment