
TIMU ya Simba SC imeanza vibaya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuchapwa bao 1-0 na Petro de Luanda ya Angola katika mchezo wake wa kwanza wa Kundi D jioni ya Jumapili ya tarehe 23 Nov 2025 Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Bao pekee lililoizamisha Simba SC limefungwa na kiungo Mreno, Bernardo Oliveira Dias dakika ya 78 alipofumua shuti la umbali wa Nita 20 ambalo lilimbabatiza beki raia wa Afrika Kusini, Rushine De Reuck na kubadili njia likimpoteza mwelekeo kipa namba moja Tanzania, Yakoub Suleiman Ali.
Mechi nyingine ya Kundi D jana Espérance ililazimishwa sare ya bila mabao na Stade Malien ya Mali Uwanja wa Hammadi Agrebi, Tunisde Jijini Tunis nchini Tunisia.
Mechi zijazo Simba SC itasafiri kuwafuata Stade Malien Novemba 29 Uwanja wa Machi 26 Jijini Bamako nchini Mali, wakati Petro de Luanda wanarejea nyumbani kuwakaribisha Espérance de Tunis November 29. Uwanja wa Novemba 11 Jijini Luanda.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment