WENYEJI, Yanga SC wameanza vyema hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya AS FAR Rabat ya Morocco jioni ya Jumamosi ya Tarehe 22 Novemba 2025 Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee katika mchezo huo wa kwanza wa Kund B, mshambuliaji wa Kimataifa wa Zimbabwe, Prince Mpumelelo Dube dakika ya 58 akimalizia pasi ndefu ya kiungo mzawa, Mudathir Yahya Abbas.
Hii inakuwa mara ya kwanza kihistoria Yanga kushinda mechi ya kwanza ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika wakiposhiriki kwa mara ya kwanza mwaka 1998.



Tupe maoni yako

0 comments:
Post a Comment