ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 23, 2025

TAZAMA HAPA MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2024

 

Bofya Hapa chini kutazama matokeo




Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya Kidato cha Nne kwa mwaka 2024, ambapo watahiniwa 477,262 kati ya wanafunzi 516,695 wenye matokeo wamefaulu kwa kupata madaraja ya I, II, III na IV.

NECTA imesema ufaulu huo umepanda kwa asilimia 3, hivyo kufikia asilimia 92.37 kutoka asilimia 89.36 mwaka 2023.

Aidha kwa mwaka 2024, takwimu zinaonesha idadi ya watahiniwa waliopata madaraja ya I, II na III imeongezeka na kufikia 221,953 sawa na asilimia 43, ikilinganishwa na mwaka 2023 ambapo idadi ilikuwa  197,426 sawa na asilimia 37.4.

Idadi ya watahiniwa waliopata daraja la IV na zero imepungua, hivyo ubora wa ufaulu umepanda kwa asilimia 5.6.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.