ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 3, 2022

MWILI WA KICHANGA WAOKOTWA KWENYE DAMPO LA SOKO

 


WAKAZI wa mtaa wa Shibayi kata ya Buhongwa wilayani Nyamagana jijini Mwanza wamekumbwa na taharuki baada ya kuona mwili wa kichanga kinachokadiriwa kuwa na umri wa miezi sita ukiwa umewekwa kwenye boksi na kutupwa katika dampo lililopo kwenye soko la mtaa huo. 

Mwili huo unadaiwa kutupwa leo majira ya mapema asubuhi kwenye dampo ambapo watu waliokuwa wanaokota mabaki ya chakula waliustukia mwili huo wakati wakisakura moja ya mamoksi ambapo hatimaye walinasa mwili huo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.