ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 30, 2021

TAARIFA YA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM MAALUM ILIYOKETI JULAI 29,2021,Ikulu Jijini Dar es Salaam

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiongoza Kikao Maalum cha Kamati Kuu  ya Chama cha Mapinduzi CCM kilichokutana leo Julai 29,2021 Ikulu jijini Dar es salaam.



Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiongoza Kikao Maalum cha Kamati Kuu  ya Chama cha Mapinduzi CCM kilichokutana  Julai 29,2021 Ikulu jijini Dar es salaam.



 Wajumbe wa Kamati kuu wakifuatilia Kikao  Maalum cha Kamati Kuu  ya Chama cha Mapinduzi CCM kilichokutana  Julai 29,2021 Ikulu jijini Dar es salaam. (PICHA NA FAHADI SIRAJI WA CCM)

 Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa imekutana katika kikao maalumu Alhamisi 29 Julai, 2021 Ikulu Jijini Dar es Salaam chini ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Samia Suluhu Hassan.


Pamoja na mambo mengine Kamati Kuu imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wa kuruhusu chanjo ya virusi vya ugonjwa wa korona (UVIKO 19) Kutolewa nchini na yeye kuwa mfano wa  kukubali kuchanjwa ikiwa ni udhibitisho wa usalama wa chanjo hiyo. 

Uamuzi wake umetajwa kuwa ni kielelezo cha upendo na uzalendo mkubwa alionao katika kujali afya za watanzania na ni hatua nzuri ya Tanzania kuungana na dunia katika kukabiliana dhidi ya UVIKO-19, pia ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020 - 2025 Ibara ya 83(o) na 84.

Kamati Kuu imeelekeza kuanza kuchukuliwa hatua kwa wale wote wanaokiuka mienendo, taratibu na kanuni za maadili na uongozi kwa mujibu wa katiba ya Chama Cha Mapinduzi.

Aidha Kamati Kuu imefanya uteuzi wa makatibu wakuu wa Jumuiya za Chama Cha Mapinduzi ambapo Ndugu Gilbert Kalima Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania na Dkt. Philis Nyimbi Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania  (UWT).


Shaka Hamdu Shaka
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
Itikadi na Uenezi
29 Julai, 2021.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.