ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 22, 2017

MAMA SALMA KIKWETE KUZINDUA KAMPENI YA KAMBI YA WANAFUNZI WA MASOMO YA SAYANSI MKOANI IRINGA




Wanafunzi wa shule za sekondari manispaa ya iringa kunufaika na elimu ya masomo ya sayansi kutokana na kuandaliwa kambi maalumu kwa ajili ya kuwafindisha kutoka kwa walimu waliobobea katika masomo hayo kwa wanafunzi wa watakao kuwa tayari kupata elimu hiyo.

Ofisi ya mbunge wa viti maalum Ritta Kabati imeandaa mpango wa kuwaongezea elimua wanafunzi wa shule za sekondari manispaa ya Iringa kwa kuanzisha kambi ya masomo ya sanyasi itakayo kuwa inafanyika bure kwa wanafunzi wa watakao kuwa tayari kupata elimu hiyo.

Akizungumza na Nuru fm Dicksoni Kawovela ambaye ni mratibu wa miradi ya jamii kutoka ofisi ya mbunge RITTA KABATI amesema kuwa wameamua kuja na mpango huo kwa lengo la kuinua elimu ya sayansi kwa wanafunzzi wa shule za sekondari hapa manispaa.

Aidha Kawovela amesema kuwa mafunzo hayo yatakuwa na manufaa kwa walimu na wanafunzi watakaokuwa wanahudhuria masomo haya ambayo yatakuwa yanatolewa bure.

Kawovela amewaka wazazi wa wanafunzi kuwaruhusu watoto wao kwenda kwenye makambi hayo ili waongezewe uwezo katika masomo ya sayansi.

Hata hiyo Kawovela alisema kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo atakuwa mama Salma Kikwete ambaye ni mbunge wa kuteuliwa na Rais katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.