ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 22, 2016

AMANA BANK TANZANIA WAZINDUA KITUO CHA HUDUMA KWA WATEJA

Juma Msabaha ambaye ni senior costomer service manager wa Bank Ya AMANA nchini Tanzania akifafanua jambo kwa wanahabari wakati Bank Hiyo ikizindua Rasmi Kituo cha Huduma kwa wateja ambacho ni mahsusi kwa kuwasaidia wateja wake kuzifikia na kuzipata Huduma Zao kiurahisi zaidi


Benki ya kwanza ya Kiislam nchini Tanzania Amana benki leo imezindua kituo chake cha huduma kwa wateja ambacho kitakuwa kikiwasaidia wateja wake kuweza kupata taarifa mbalimbali kuhusu huduma zao kama maulizo kuhusu bidhaa za amana, Atms,huduma za mitandao (simu banking) na amana banki mtaani n.k.

Kituo hicho kitakuwa kikifanya kazi kuanzia saa 2  asubuhi mpaka saa 4 na watakuwa wanapatikana kwa nambari 0657980000 ambapo amana Bank ni miongoni mwa benki zinazofanya vizuri kwa sasa wana matawi saba matano yakiwa Dar es salaam,Arusha,Mwanza na wanatarajia kufungua matawi mengine mikoa mingi zaidi ila waliyoipa kipaumbele zaidi ni Zanzibar na Tanga

Akizungumza na waadishi wa habari meneja mfawidhi na huduma kwa wateja Juma Msabaha Amesema kuwa utaratibu wanaotumia  kuweza kuwapata mawakala ni kwamba wakala lazima awe na leseni ya biashara pia awe na tin namba ya biashara kuonyesha kuwa ni mlipa kodi  pia awe amefanya kazi zaidi ya miaka miwili na pia anaweza kuomba uwakala kwa namba zao ambazo ni 0657980000 au info@ amanabank.co.tz na maombi yake yatapelekwa BOT kuweza kujadiliwa na kama amekidhi vigezo atapewa uwakala ambapo amesema kuwa kwa sasa wana mawakala kwa mikoa kama tabora ,bukoba,na mtwara na bado wanaendelea kupokea maombi kutoka kwa watu mbalimbali.

Munir Rajab – mkuu wa idarara ya biashara amana benki amisema kuanzishwa kituo hicho kuna lengo la kuhitaji kuwa karibu na na wateja wao huku akitanabaisha  kuwa huduma za kibenki huwa zinafanana lakini kinachoweza kuwatofautisha ni ubora wa huduma kwa wateja na kwamba wao wamejipanga vizuri kuingia kwenye ushindani huo ambapo wameamua kuwa mwaka huu ni mwaka wa mawakala kwa sababu wanahitaji kuweza kuwafikia wateja wao mpaka mahali ambapo hakuna matawi na wataweza kutumia huduma za kibenki kupitia mawakala wao .
 Mkuu wa biashara wa Bank ya AMANA nchini Tanzania Munir rajab akieleza mambo mbalimbali kwa wanahabari kuhusu huduma hiyo mpya kutoka kwao
Bw. Juma Msabaha akijibu swali wa muandishi wa habari Alisema kuwa utaratibu wanaotumia  kuweza kuwapata mawakala ni kwamba wakala lazima awe na leseni ya biashara pia awena tin namba ya biashara kuonyesha kuwa ni mlipa kodi  pia aweamefanya kazi zaidi ya miaka miwili na pia anaweza kuomba uwakala kwa namba zao ambazo ni 0657980000 au info@ amanabank.co.tz na maombi yake yatapelekwa BOT kuweza kujadiliwa na kana amekidhi vigezo atapewa uwakala . na kwa sasa wana mawakala kwa mikoa kama Tabora ,Bukoba,na Mtwara na bado wanaendelea kupokea maombi kutoka kwa watu mbalimbali.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.