ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 22, 2013

TANZANIA YATINGA KWENYE KUMI BORA NDANI YA LONDON FASHION WEEK.

Wabunifu mitindo Jackline Kibacha na Anna Lukindo wakisindikizwa na Mama Balozi Joyce Kallanghe na Mama Rose Kiondo 


Nje ya Jumba la Somerset .

Wanamitindo wa Kitanzania kwenye London Fashion Week 2013. Anna Lukindo, Christine Mhando, Jacquline Kibacha 

 Mama Rose Kiondo, Samson Soboye, Mama Joyce Kallaghe, Anna Lukindo, Christine Mhando, Jacquline Kibacha 

Anna Luks 

Anna, Jack na Duane kutoka Jamaica 

Barabara ya The Strand copy

London Fashion Week 2013
-Imeandikwa na Urban Pulse na Freddy Macha
-Picha zote za Urban Pulse

Jumapili mchana  wilaya ya Westminster jijini  London ilikuwa na mashindano ya ubunifu na urembo katika maonyesho  ya kimataifa ya London Fashion Week. Mashindano haya yalifanyika jumba la Somerset lililosimama imara  kwenye upembe wa  kaskazi ya mto Thames.

Maonyesho ya London Fashion Week, bado yanaendelea jumba hili  la Somerset toka tarehe 14 hadi tarehe 28. Wiki hizi mbili nzima zitakutanisha kila mtu anaye husika na biashara ya mavazi na urembo. Magwiji na mapapa wa mitindo, wabunifu, walimbwende, watafuta vipaji, wafanya biashara, wazalishaji mali ghafi na wamiliki viwanda.  Wote hukutana katika maonyesho haya. Hapa si vipaji tu vinavyojionyesha, bali pia watu wa biashara.

Siku hii Tanzania ilikuwa moja ya nchi mbili tu za Kiafrika zilizochaguliwa na British Council na LFW kushiriki kwenye mashindano  ya kutafuta vipaji chipukizi kwenye tasnia ya ubunifu wa mavazi na urembo.  Watanzania Anna Lukindo, Jacqueline Kibacha na  Christine Mhando ndio wasanii waliobeba bendera ya taifa letu na kutuwakilisha katika mashindano haya ya kimataifa yanayofanyika kila mwaka kwa zaidi ya miaka 27 sasa.

Katika kuunga mkono maendeleo ya Tanzania na Watanzania,  Ubalozi wetu  Uingereza na Bodi ya Utalii Tanzania, nao pia walichukua nafasi hii kuwasaidia wananchi hawa kufanikisha mahitaji yao ya ushindani. Ubalozi umetoa Ukumbi wa Nyumba Ya Tanzania ulioko Bond Street ili wasanii hao waweze kuonyesha nguo na sanaa zao kwa juma zima kama sheria za London Fashion Week zinavyoamuru. Vile vile Bodi ya Utalii ya Tanzania imesaidia katika mchango  wa mali ghafi zilizotumika katika shughuli hizi  ili kuiuza Tanzania kimataifa.

Mshindi wa tukio alikua Estonia. Ingawa  Tanzania haikuwa mshindi wa mwanzo- ilichaguliwa kati ya Kumi Bora jambo ambalo limetikisa nyoyo na vichwa vya  waandaaji, wabunifu,wafanya biashara na watafuta vipaji vya kimataifa. Hii ni mara ya kwanza kwa taifa letu kushiriki katika shughuli na  wote wameguswa na kupumbazwa na usanii wa hali ya juu ulioonyeshwa na wasanii  watatu wa Kitanzania.   Lukindo, Mhando na Kibacha wamechukua nafasi waliyopewa kwa mikono miwili na wote wameisogeza Tanzania hatua moja zaidi ndani ya ulingo wa kimataifa na katika biashara hii ya mavazi na urembo ambayo inasemekana ina thamani ya  Pauni Billioni 10  ama  shilingi Trillion 25 za Tanzania.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.