ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, May 13, 2024

YANGA BINGWA TENA. SASA NI MARA 30.

  


LIGI Kuu ya NBC Tanzania bara ikiendelea tena leo Mei 13, 2024 huku macho na masikio yakielekezwa katika dimba la Manungu Complex, Turiani Morogoro ambapo Wananchi wametawazwa  kuwa Mabingwa wa Ligi Kuu kwa mara ya 30 kihistoria baada ya  ushindi wa goli 3-1 wakizoa pointi dhidi ya Wakata Miwa.


Yanga Sc wamefikisha alama 71 ambazo hazitafikiwa na timu yoyote kwa mechi zilizosalia kabla ya kufungwa kwa pazia la Ligi.

Azam Fc waliopo nafasi ya pili wakishinda mechi tatu zilizosalia watafikisha pointi 69 sawa na Simba Sc ambao watafikisha pointi 69 wakishinda michezo yao minne iliyobaki.

MSIMAMO 🔝3️⃣
🥇Yanga Sc — mechi 27 — pointi 71
🥈 Azam Fc — mechi 27 — pointi 60
🥉 Simba Sc — mechi 26 — pointi 57

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.