ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, September 26, 2023

WIZARA YA MADINI KURUSHA NDEGE YA UTAFITI NCHI NZIMA 'MADINI NI MAISHA NA UTAJIRI'

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

"Utajiri wa Sekta ya Madini ni taarifa hakuna uchawi mwingine wowote" 'MADINI NI MAISHA NA UTAJIRI' fuatilia ufafanuzi wa kauli hii kutoka kwa Waziri wa Madini Mhe. Anthony Peter Mavunde (mbunge) aliyoitoa katika 'Kikao Kazi' cha Waziri huyo na Menejimbenti ya Tume ya Madini, kilichofanyika katika ukumbi wa BOT jijini Mwanza leo Tarehe 26 September 2023. "Unayoyaona yote haya kama matunda ya sekta hii yanatokana na eneo dogo sana lililofanyiwa utafiti, tumejiwekea malengo ifikapo mwaka 20230 tuwe tumelipitia eneo la nchi nzima kwaajili ya kufanya utafiti na tupate viashiria vya madini mengine tofauti tofauti ili tuongeze wigo na mchango wa Sekta hii katika uchumi wa Tanzania" alisema Waziri Mavunde na kuongeza "Tumedhamiria tutakwenda kufanya utafiti wa kina kwa kurusha ndege, helkopta na drones kupata picha za miamba yote kwa maeneo yote nchini yaani kufanya HIGH-RESOLUTION GEOPHYSICAL (HRG) SURVEYS ambayo itatupa picha kama hatua ya awali ya viashiria ili baadaye tuendelee na shughuli za uchorongaji na kuweza kubaini madini tuliyonayo" alisema Waziri Mavunde na kuongeza "Lakini hatua ya kwanza ni ya upigaji wa picha" #jembefm #samiasuluhuhassan #kaziiendelee #mwanza #mavunde

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.