ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 16, 2023

MWANAMKE AMKIRI BABAKE NI MZAZI HALISI WA WATOTO WAKE 3 WALA SI MUMEWE.


Mwanamke mmoja kutoka Ghana amesimulia hadithi yake tata ya mapenzi katika barua ambayo haikutajwa jina lake kwa kipindi maarufu cha uhusiano cha Citi FM/Citi cha Sister Sister.

Kulingana na mwanamke huyo kutoka Ghana, ameolewa na mume wake kwa miaka mingi na walijaliwa watoto watatu warembo lakini ukweli ni kwamba, hakuna mtoto ambaye ni wa mwanamume huyo. "Babangu huwa ananipeleka likizo, lakini mume wangu huwa halalamiki kwa sababu haoni ubaya. Nina umri wa miaka 35 sasa, nina watoto watatu warembo, na wote ni wa babangu, lakini hakuna mtu aliyewahi kushuku kwa sababu ninamfanana," alisema katika barua hiyo.

Mwanamke huyo alisema amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na baba yake kwa miongo kadhaa, lakini sasa anaanza kuhisi vibaya.

 

Hadithi yake iliwashtua wengi mitandaoni na baadhi walikuwa na haya ya kusema:

 Ama Marfo alisema: "Baba yako? Watoto watatu! Wote wawili mko kwake kweli mna pepo. Mnamhitaji Yesu. Tafadhali mwache mume wako asiye na hatia nje ya laana hii."

Jackie Alex  alisema: "Siamini nilichokisoma!"

Akua Twumwah alitoa maoni yake: "Omba talaka. Inakuwaje nyinyi wawili mnafanya hivyo, si hii wanaiita dhambi au tuitaje?"

 Agnes Sarkodee-Adoo Tekyi alisema: "Tamaa ni kubwa na mahusiano haya ya kifamilia yanazidi kuendelea. Ungepaswa kuacha hili tangu mwanzo. Mungu aturehemu jamani."

 Racheal Muliwa alisema: "Maajabu haya! Babako wa kukuzaa, na wewe bado uko katika ndoa!!! Kuzaa watoto na babako!!! Wewe umelaaniwa."

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.