ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 9, 2023

"MUME ALIRUDI SAA SABA USIKU MWANAMKE AUA WATOTO WAKE WAWILI, KUMCHOMA VISU MUME WAKE MARA TATU KISHA KUJARIBU KUJIUA


Polisi wanachunguza kisa ambapo mwanamke mmoja anadaiwa kuua watoto wake wawili, Kumchoma visu mume wake mara tatu kabla ya kujaribu kujiua eneo la Ongata Rongai.

Mwanamke huyo ambaye amelazwa katika Hospitali Kuu ya Kenyatta na akiwa hali mahututi, anasemekana kumchoma visu  mume wake kufuatia ugomvi katika nyumba yao kwenye barabara ya Maasai Lodge.

Ugomvi huo ulielekea pabaya baada ya mwanamke huyo kumdunga mume wake mara tatu – kichwani,shingoni - baada yake kurejea nyumbani saa saba usiku, polisi wanasema.

Mwanamume huyo alinusurika kifo baada ya kukimbia kutoka kwa nyumba hiyo akibubujikwa na damu na kuomba msaada kutoka kwa majirani ambao walimkimbiza kwenye kituo cha afya kilicho karibu

Kwa mujibu wa polisi, mama huyo wa watoto wawili ambaye alibaki nyumbani, anasemekana kufunga milango kabla ya kuua wanawe wawili - miaka sita na miwili – kuwachoma visu.

Polisi wanasema kuwa alijaribu kujiua kwa kisu hicho lakini juhudi zake ziliambulia patupu.

 Alisalia na vidonda kwenye tumbo na kifua.

Polisi waliitwa eneo la tukio na kupeleka miili hiyo kwenye hifadhi ya maiti.

Wanandao hao wamelazwa hospitalini chini ya ulinzi mkali. Kamanda wa Polisi wa Kajiado Kaskazini Hussein Gura alisema kuwa polisi walipata silaha iliyoyumiwa kutekeleza mauaji hayo na wameanzisha uchunguzi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.