ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 4, 2023

PIKIPIKI YALIPUKA NA KUTEKETEA JIJINI MWANZA.


 Pikipiki ambayo jina la mmiliki wala namba zake hajafahamika mara moja imelipuka na kuteketea kwa moto katika tukio lililotokea eneo la kituo cha mabasi madogo ya Posta jijini Mwanza.

Akizungumza na Mwananchi muda mfupi baada ya pikipiki hiyo ambayo hata dereva wake hakufahamika, Faustine Magiri, mmoja wa mashuhuda amesema kabla ya kulipuka moto, pikipiki hiyo iliyokuwa ikitokea njia ya Nyegezi kupitia barabara kuu ya Kenyatta ilikuwa ikivuja mafuta ambayo yaliacha michirizi barabarani.

“Pikipiki ile iliwaka moto na kuanza kuteketea likiwa bado linatembea ndipo dereva akalisimamisha na kuruka kuepuka kuungua,” amesema Faustini Magiri, anayemiliki duka la vifaa vya ujenzi karibu na eneo la tukio

Amesema pikipiki hiyo ilishika moto wakati dereva wake alipokuwa akielekea kwenye duka lake ndipo alipompigia kelele kumgutusha ashuke asiungue.

"Tulivyofuatilia, tuligundua pikipiki ile ilikuwa ikimwaga mafuta na kwa bahati mbaya dereva hakushtuka hadi ilipolipuka na kuteketea,” amesema Magiri

Amesema kukosa elimu na uelewa mpana wa namna ya kukabiliana na majanga ya moto ndio kumesababisha pikipiki hiyo kuteketea kwa sababu licha ya watu kujitokeza mapema, hakuna aliyeweza kusaidia kuzima moto huo.

“Mmoja wa wananchi alikuja nan doo ya maji na kumwagia pikipiki iliyokuwa ikiteketea; badala ya kuzimika, moto ukaongezeka mara dufu. Wananchi wangekuwa na elimu ya kutosha ya kukabiliana na majanga ya moto wangetumia mchanga au blanketi kufunika pikipiki ile kupunguza hewa ya Oksijeni ili moto uzimike,’’ amesema Hellene Zablon, mjasiriamali anayeuza mihogo ya kukaanga eneo la Posta

Juma Masanja, mmoja wa wafanyabiashara ndogo ndogo maarufu kama Machinga amewashauri wamiliki na madereva wa vyombo vya moto kujenga utamaduni wa kukagua vyombo vya kujiridhisha na ubora na usalama kabla na baada ya safari.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.